Wednesday, March 5, 2014

IMG_4521Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe, Dar es salaam
Tel: 0712461976/0764302956
WEKUNDU wa msimbazi Simba “Taifa kubwa” wameanza mazoezi katika uwanja wa Kinesi jijini Dar es salaam chini ya kocha wake mkuu, Mcroatia Dravko Logarusic, kujiwinda na mtanange wa vuta ni kuvute dhidi ya Maafande wa Tanzania Prisons “wajelajela” katika dimba la sokoine jijini Mbeya jumapili machi 9 mwaka huu.
Afisa habari wa Simba, Asha Muhaji ameuambia mtandao huu kuwa baada ya mechi ya jumapili dhidi ya Ruvu Shooting waliyoshinda mabao 3-2, waliwapa mapumziko ya siku moja wachezaji wao ili kujipanga na maandalizi ya mechi ijayo.
“Sisi tuna utaratibu wa kuwapumzisha wachezaji wetu kwa siku moja baada ya mechi, hivyo jumatatu hawakuwa na mazoezi, na hapo jana wameanza mazoezi kinessi na watakuwa hapo mpaka siku ya safari yetu kuelekea Mbeya”. Alisema Muhaji.

Na Saleh Ally, Cairo
Mabingwa wa Afrika, Al Ahly ya hapa, wameamua kuondoka kwenye uwanja ambao wamekuwa wakifanyia mazoezi na kujichimbia kusikojulikana.
Al Ahly wameamua kufanya hivyo ili kufanya maandalizi yao kwa utulivu kabla ya kuivaa Yanga katika mechi ya marudiano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Jumapili.
Katika mechi ya kwanza jijini Dar es Salaam mabingwa hao wa Afrika walilala kwa bao 1-0 lililofungwa na nahodha wa Yanga, Nadir Haroub 'Cannavaro' na kwa mara ya kwanza Yanga ikafuta uteja wa kufungwa kila inapokutana na Al Ahly.
Lakini mashabiki wao wengine wameeleza kuwa Ahly wameamua kujichimbia kutokana na vurugu zilizofanywa na mashabiki wake mara baada ya kupata taarifa kuwa wamefungwa bao 1-0 jijini Dar es Salaam.
"Wakati mwingine imekuwa kawaida Ahl kuondoka na kujificha sehemu kwa ajili ya maandalizi, lakini safari hii mambo yamekuwa tofauti kidogo, wanaonyesha wmepania kushinda mechi hii.
"Tokea wamerudi hawajaonekena klabu, huenda ni hofu ya mashabiki waliokuja kufanya vurugu hapa wakipinga wao kufungwa na timu kutoka Afrika Mashariki, lakini pia suala la umakini tu," alisema mmoja wa wafanyakazi kwenye uwanja huo kwa Kingereza cha tabu.
Championi lilifunga safari hadi kwenye uwanja huo jana mapema kutaka kushuhudia mazoezi yao, lakini likaambulia patupu na kuelezwa hivi: "Hutamuona mtu hadi siku ya mechi."
SOURCE: CHAMPIONI NEWPAPER (P.T)

140304202811_ukraine_soldiers_512x288_afp_3a8b7.jpg
Hali ya wasiwasi imekumba jimbo la Crimea.
Rais Obama ametangaza mapendekezo ambayo huenda yakatoa suluhu kwa mzozo wa Ukraine, ikiwemo kuwatuma wachunguzi wa kimataifa na kuanzishwa mazungumzo ya moja kwa moja kati ya Moscow na serikali mpya mjini Kiev.
Bwana Obama amejadili swala hilo kwa njia ya simu na chanzela wa Ujerumani, Angela Merkel.
Wachunguzi hao watalenga kulinda haki za watu wa kabila la Urusi waliopo katika jimbo la Crimea; na kwa upande wake Urusi itahitajika kuwaondoa wanajeshi wake katika jimbo hilo. Pendekezo hilo huenda likajadiliwa pembezoni mwa mkutano utakaofanyika nchini Ufaransa (Jumatano) ambao utawaleta pamoja wajumbe kutoka Marekani, Urusi na kwingineko kwa ajili ya kuijadili Lebanon.
Hapo awali waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Marekani John Kerry, amelaani kile amekitaja kuwa kitendo cha uchukozi kutoka Urusi dhidi ya Ukraine. Wakati wa ziara yake mjini Kiev ambapo aliweka shada la maua kuwakumbuka waandamanaji waliouwawa mwezi uliopita, bwana Kerry ameshutumu Moscow kwa kutumia uongo na vitisho kuficha ukweli.
Mwandishi wa BBC Sarah Reinsford aliyepo mjini Kiev amesema kuwa wakati akiweka shada la maua katika maeneo walikouwawa mamia ya waandamanaji mjini humo, John Kerry alikaribishwa na umati wa watu waliokuwa wakiomba msaada wa marekani.
Na hilo ndilo lililomleta hapa; kutoa msaada wa hali na mali na pia wa kisiasa kwa serikali ya mpito ya Ukraine, na pia ahadi ya msaada wa kifedha na wa kiufundi kusaidia katika kuimarisha uchumi, amesema mwandishi wetu.
140304180342_putin_press_conference_304x171__nocredit_2b529.png
Rais Putin.
Lakini zaidi ya yote bwana Kerry ameleta ujumbe kwa Moscow.
" Nadhani ni bayana kwamba Urusi imekuwa ikifanya bidii kubuni dhana ya kuiwezesha kutekeleza uvamizi zaidi. Urusi imezungumzia raia wachache wanaozungumza kirusi ambao wamezingirwa. Ukweli ni kwamba hawajazingirwa! Ukweli ni kwamba serikali mpya ya Ukraine imewajibika ipasavyo kwa kuhimiza utulivu na kujiepusha na uchokozi," amesema Bwana Kerry.
Haukuna ushahidi, amesisitiza, kwa madai ya urusi kwamba wanajeshi wake wanalinda raia wanaozungumza lugha ya kirusi nchini Ukraine akiishutumu moscow kwa kutumia uongo na vitisho kuficha ukweli.
Katika karne ya ishirini na moja, bwana Kerry ameonya, haiwezekani kuvamia taifa jingine na kisha kuamrisha matakwa yako yatekelezwe kwa kutumia mtutu wa bunduki. Na kisha akamhimiza rais Putin kuwaondoa wanajeshi wake katika jimbo la Crimea na kushughulikia malalamishi yake kupitia njia za kisheria na amani.
Lau sivyo, ameonya, kwamba Urusi itakabiliwa na vikwazo zaidi vya kiuchumi na kisiasa.

waliotembelea blog