Wednesday, March 5, 2014

IMG_4521Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe, Dar es salaam
Tel: 0712461976/0764302956
WEKUNDU wa msimbazi Simba “Taifa kubwa” wameanza mazoezi katika uwanja wa Kinesi jijini Dar es salaam chini ya kocha wake mkuu, Mcroatia Dravko Logarusic, kujiwinda na mtanange wa vuta ni kuvute dhidi ya Maafande wa Tanzania Prisons “wajelajela” katika dimba la sokoine jijini Mbeya jumapili machi 9 mwaka huu.
Afisa habari wa Simba, Asha Muhaji ameuambia mtandao huu kuwa baada ya mechi ya jumapili dhidi ya Ruvu Shooting waliyoshinda mabao 3-2, waliwapa mapumziko ya siku moja wachezaji wao ili kujipanga na maandalizi ya mechi ijayo.
“Sisi tuna utaratibu wa kuwapumzisha wachezaji wetu kwa siku moja baada ya mechi, hivyo jumatatu hawakuwa na mazoezi, na hapo jana wameanza mazoezi kinessi na watakuwa hapo mpaka siku ya safari yetu kuelekea Mbeya”. Alisema Muhaji.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog