Thursday, September 11, 2014

ENGLAND: Premier League
04:45 Arsenal-Manchester City


07:00 Chelsea-Swansea


07:00 Crystal Palace-Burnley


07:00 Southampton-Newcastle Utd


07:00 Stoke City-Leicester


07:00 Sunderland-Tottenham


07:00 West Brom-Everton


09:30 Liverpool-Aston Villa


Liverpool


Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
KOCHA mkuu wa Mbeya City fc na kocha bora wa ligi kuu Tanzania bara msimu uliopita, Juma Mwambusi, amewakaribisha makocha Patrick Phiri wa Simba na Marcio Maximo wa Yanga.
Akizungumza mchana huu na MPENJA BLOG, Mwambusi amesema kocha Phiri ana historia ya kufundisha soka la Tanzania kwa ngazi ya klabu wakati Maximo amefundisha timu ya Taifa, lakini wote wataleta changamoto nzuri kwake.
Mwambusi aliongeza kuwa ujio wa makocha wapya unaleta vionjo vipya katika ligi, lakini yeye kama mwalimu anajipanga kukabiliana kwa nguvu zote ili kuendeleza mafanikio ya msimu uliopita.
“Mimi naona tungoje dakika 90 zitakuwa zinatoa majibu. Sina la kusema zaidi ya kusema ni changamoto. Mwalimu mpya anapopatikana katika ligi anakuja na kionjo kipya, kama mwalimu lazima ukabiliane nacho. Kwahiyo sisi tunawakaribisha ligi kuu Phiri na Maximo.” Alisema Mwambusi.
Aidha, Mwambusi alifafanua kuwa maandalizi ya ligi kuu yanakwenda vizuri  na wapo hatua za mwisho kabisa kuhakikisha wanapata kikosi cha kwanza.
Alisema mwishoni mwa wiki hii wanatarajia kupata mechi ya mwisho ya kirafiki itakayofunga mahesabu ya kuanza msimu mpya unaotarajia kuanza septemba 20 mwaka huu.
“Vijana wanaendelea vizuri na tuko katika kumalizia-malizia maandalizi na tunaangalia utaratibu wa kupata timu ya kucheza mechi ya kirafiki ili kupata kikosi cha kwanza”
“Wachezaji wote wako katika hali nzuri, kikubwa tunadhani mwishoni mwa wiki hii tutakuwa na mechi ya kirafiki ambayo itakamilisha maandalizi yetu na tujue tunatokaje katika mechi za ligi kuu.”
“Bado viongozi wanafanya jitihada  kupata timu kutoka Malawi na ikishindikana tutacheza na timu ya hapa ndani ambayo itatupa upinzani mzuri”
 Kocha huyo maarufu kwa sasa alisema soka sio mchezo wa kutabiri, lakini anashukuru kwa vile mwaka jana walitoa changamoto kubwa na timu nyingi zinataka kuwaiga wao.
“Mpira wa miguu sio wa kutabiri, lakini mimi nashukuru kwa kuwa mwaka jana Mbeya City fc tumeleta changamoto na watu wanajiandaa vizuri sana na kila mtu anataka kuona timu yake itafanyeje ili iweze kuwa kama Mbeya City. Mimi nafikiri ligi itakuwa na changamoto sana mwaka huu.
Msimu uliopita, Mbeya City ilishika nafasi ya tatu kwa pointi 49 nyuma ya Yanga walioshika nafasi ya pili na Azam fc nafasi ya kwanza (mabingwa).

Mbeya city wanatarajia kuanza kampeni zao za kusaka ubingwa msimu wa 2014/2015 septemba 20 mwaka huu  katika uwanja wa nyumbani wa Sokoine jijini Mbeya dhidi ya maafande wa JKT Ruvu.


Issa Rashid (kulia)
BEKI wa Simba Issa Rashid ‘Baba Ubaya’ atalazimika kukaa nje ya uwanja kwa wiki mbili baada ya kuumia nyama za paja kwenye moja ya mazoezi ya klabu hiyo, daktari wa Simba, Yassin Gembe amethibitisha.
Mbali na beki huyo straika Elius Maguli alilazimika kupumzishwa kufanya mazoezi na wachezaji wengine baada ya kuugua Malaria ambapo mpaka jana Jumatano mchana haikufahamika mara moja kuwa angerejea kuendelea na programu hizo siku gani.
Gembe alisema baada ya kwenda kumfanyia vipimo Jumatatu ya wiki hii, Baba Ubaya alishauriwa kukaa nje kwa muda wa wiki mbili wakati Maguli alipumzisha juzi Jumanne kufanya mazoezi na wachezaji wenzake kutokana na kusumbuliwa na Malaria.
“Baba Ubaya atalazimika kukaa nje kwa wiki mbili kuanzia leo (Jumanne) baada ya kugundulika kuwa majeraha yake ya nyama za paja si madogo kama tulivyodhani mwanzo,” alisema Gembe
Majeraha hayo yatamfanya Baba Ubaya kuukosa mchezo wa ufunguzi wa Ligi kati ya Simba na Coastal Union utakaochezwa Jumapili ya Septemba 21.
Chanzo: Mwanaspoti



MCHEZAJI wa Simba Willium Lucian ‘Gallas’ amebadilisha nafasi katika kikosi cha Simba kutoka beki wa kulia alikokuwa akicheza awali na kupelekwa kucheza kama kiungo mkabaji kikosini hapo.
Kocha wa Simba, Mzambia Patrick Phiri ameamua kumbadilisha Gallas na kumpeleka katikati baada ya kugundua kuwa beki huyo mbali na uwezo wa kucheza kama beki wa kulia pia anaweza kucheza kama beki wa kati ama kiungo mkabaji.
Mabadiliko hayo yamechagizwa zaidi na kuumia kwa kiungo Jonas Mkude, ambaye ameiacha nafasi hiyo ya kiungo chini ya Mrundi Pierre Kwizera pekee. Said Ndemla na Abdallah Seseme ambao wanaweza kucheza katika nafasi hiyo si wazuri katika kukaba jambo lilimfanya Phiri kufanya maamuzi hayo.
Mkude aliumia alipokuwa na Taifa Stars nchini Botswana mapema Julai mwaka huu na kulazimika kukaa nje kwa zaidi ya miezi miwili. Taarifa kutoka kwa daktari wa Simba, Yassin Gembe ni kwamba Mkude atarejea rasmi uwanjani Oktoba 12.
“Ni kweli nimeamua kumpeleka Gallas katikati, ni mzuri anapocheza hapo kwani anajua kukaba lakini pia anaweza kucheza kama beki wa pembeni na kati, ni mchezaji mzuri,” alisema Phiri.
Katika mchezo dhidi ya Gor Mahia Jumamosi iliyopita, Gallas alichezeshwa katika nafasi hiyo ya kiungo na kucheza kwa ustadi kabla ya kufanyiwa mabadiliko katika kipindi cha pili.


Manchester United sold Danny Welbeck to rivals Arsenal for £16million after the arrival of Radamel Falcao
Manchester United walimuuza Danny Welbeck kwa wapinzani wao wakubwa Arsenal baada ya kumsaini Radamel Falcao.

GARY Neville ameishutumu sera ya usajili ya Manchester United baada ya kudai kuwa alishangazwa na kitendo cha kumuuza Danny Welbeck kwa paundi milioni 16 tu.
United walitumia fedha nyingi majira ya kiangazi kwa kumsajili Falcao, Angel di Maria, Daley Blind, Ander Herrera, Luke Shaw na Marco Rojo.
Neville alisema: "Sikutarajia kama United wangefanya biashara kama hiyo, nalidhani wangefanya zaidi ya hapo"
"Siwezi kusema sana, wiki iliyopita nilifanya kazi na Danny Welbeck  (akiwa na England), hakika ni ajabu. Nakiri wazi kuwa kumuuza Danny Welbeck ni ajabu, lakini ni kwa upande wangu".
"Kwa pesa zote walizotumia majira ya kiangazi, kuna mabeki wa kushoto na kulia walionunuliwa kwa paundi milioni 14, 16, 16?
"Arsenal walimpaje Welbeck kwa paundi milioni 16? Sielewi. Wamewasaidia wapinzani kwasababu Arsenal watakuwa wanapambana kusaka nafasi nne za juu"
"Napata shida kupata logiki, lakini sielewi, inashangaza kwa namna moja ama nyingine".
"Falcao aliingia pale, ilimshangaza kila mtu. Inaingiaje kwenye timu, sijui. Tayari walikuwa na  Rooney, Di Maria, Robin van Persie, Falcao, Herrera, Januzaj na Mata  katika timu.
Arsene Wenger alimsajili  Danny Welbeck baada ya mshambuliaji wake chaguo la kwanza Olivier Giroud kuumia
Radamel Falcao alijiunga Manchester United kwa mkopo wa Muda mrefu.

Neville aliendelea kudai kuwa United imelipa hela nyingi zaidi kwa wachezaji baada ya kushika nafasi ya saba msimu uliopita.

PosTeamPWDLGFGAGDPts
1Chelsea330011479
2Swansea City33006159
3Aston Villa32103127
4Manchester City32015236
5Liverpool32016426
6Tottenham Hotspur32015326
7Arsenal31205415
8Southampton31114314
9Hull City31113304
10Stoke City31112204
11West Ham United310245-13
12Queens Park Rangers310215-43
13Sunderland302134-12
14Manchester United302123-12
15Leicester City302135-22
16Newcastle United302135-22
17Everton3021710-32
18West Bromwich Albion302125-32
19Crystal Palace301258-31
20Burnley301214-31

waliotembelea blog