Thursday, September 11, 2014



MCHEZAJI wa Simba Willium Lucian ‘Gallas’ amebadilisha nafasi katika kikosi cha Simba kutoka beki wa kulia alikokuwa akicheza awali na kupelekwa kucheza kama kiungo mkabaji kikosini hapo.
Kocha wa Simba, Mzambia Patrick Phiri ameamua kumbadilisha Gallas na kumpeleka katikati baada ya kugundua kuwa beki huyo mbali na uwezo wa kucheza kama beki wa kulia pia anaweza kucheza kama beki wa kati ama kiungo mkabaji.
Mabadiliko hayo yamechagizwa zaidi na kuumia kwa kiungo Jonas Mkude, ambaye ameiacha nafasi hiyo ya kiungo chini ya Mrundi Pierre Kwizera pekee. Said Ndemla na Abdallah Seseme ambao wanaweza kucheza katika nafasi hiyo si wazuri katika kukaba jambo lilimfanya Phiri kufanya maamuzi hayo.
Mkude aliumia alipokuwa na Taifa Stars nchini Botswana mapema Julai mwaka huu na kulazimika kukaa nje kwa zaidi ya miezi miwili. Taarifa kutoka kwa daktari wa Simba, Yassin Gembe ni kwamba Mkude atarejea rasmi uwanjani Oktoba 12.
“Ni kweli nimeamua kumpeleka Gallas katikati, ni mzuri anapocheza hapo kwani anajua kukaba lakini pia anaweza kucheza kama beki wa pembeni na kati, ni mchezaji mzuri,” alisema Phiri.
Katika mchezo dhidi ya Gor Mahia Jumamosi iliyopita, Gallas alichezeshwa katika nafasi hiyo ya kiungo na kucheza kwa ustadi kabla ya kufanyiwa mabadiliko katika kipindi cha pili.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog