Thursday, September 11, 2014


Issa Rashid (kulia)
BEKI wa Simba Issa Rashid ‘Baba Ubaya’ atalazimika kukaa nje ya uwanja kwa wiki mbili baada ya kuumia nyama za paja kwenye moja ya mazoezi ya klabu hiyo, daktari wa Simba, Yassin Gembe amethibitisha.
Mbali na beki huyo straika Elius Maguli alilazimika kupumzishwa kufanya mazoezi na wachezaji wengine baada ya kuugua Malaria ambapo mpaka jana Jumatano mchana haikufahamika mara moja kuwa angerejea kuendelea na programu hizo siku gani.
Gembe alisema baada ya kwenda kumfanyia vipimo Jumatatu ya wiki hii, Baba Ubaya alishauriwa kukaa nje kwa muda wa wiki mbili wakati Maguli alipumzisha juzi Jumanne kufanya mazoezi na wachezaji wenzake kutokana na kusumbuliwa na Malaria.
“Baba Ubaya atalazimika kukaa nje kwa wiki mbili kuanzia leo (Jumanne) baada ya kugundulika kuwa majeraha yake ya nyama za paja si madogo kama tulivyodhani mwanzo,” alisema Gembe
Majeraha hayo yatamfanya Baba Ubaya kuukosa mchezo wa ufunguzi wa Ligi kati ya Simba na Coastal Union utakaochezwa Jumapili ya Septemba 21.
Chanzo: Mwanaspoti

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog