Sunday, September 14, 2014


Na Father Kidevu Blog
Wanyange 30 wanao wanbia taji la Redd's Miss Tanzania 2014 leo wameingia kambini tayari kwa safari ya fainali za Miss Tanzania 2014 zitakazo fanyikia mapema mwezi Oktoba jiji Dar es Salaam.
Warembo hao waliowasdili kwa muda tofauti kuanzaia saa 12 alfajiri ya leo na kupokelewa na waandaaji wa Miss Tanzania katika hoteli ya JB Belmont iliyopo katikati ya jiji la maraha la Dar.
Warembo kutoka Kanda ya Ziwa walitia fora pale warembo hao walipowasili kambini hapo wakiwa ndani ya gari ya Mshindi wa Kanda ya Ziwa ambayo alizawadiwa hivi kjaribuni katika shindano lao.


Warembo wakiwasili kambini


Warembo wa Kanda ya Ziwa wakiteremka katika gari lao baada ya kuwasili na inaelezwa waliendesha kutoka jijini Mwanza.

Warembo wa Kanda ya Ziwa wakijiandikisha baada ya kuwasili kambini.

Warembo wakielekea chumba cha mkutano.


Warembo wakiwa katika chumba cha semina ambapo maelezo mbalimbali ya ka,mbi yao yalitolewa.


Warembo wakiwa katika chumba cha semina ambapo maelezo mbalimbali ya ka,mbi yao yalitolewa.

Wadhamini wakijitambulisha kwa warembo na wanahabari.

Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania, Hasim Lundenga 'Anko' (kushoto) akiteta jambo na Katibu wake Bosco Majaliwa 'Mshua'.



Chakula cha mchana kwa warembo.


Na baraka Mbolembole, Dar es Salaam,
Salum Telela alifunga bao pekee kwa kuunganisha krosi ya mshambulizi Didier Kavumbangu na kuisaidia timu yake kupata ushindi wa bao 1-0 katika mchezo wa Ngao ya Jamii, mwaka uliopita.. Kelvin Yondan, Nadir Haroub, Saimon Msuva, ni wachezaji pekee ambao wanaweza kuanza moja kwa moja katika kikosi cha kwanza cha Mwalimu, Marcio Maximo. Mfungaji wa mwaka uliopita Telela na mlinzi wa kulia Juma Abdul ambao wote walianza katika mchezo wa ushindi mwa jana, mmoja wao atasubiri katika benchi ili kupisha utitiri wa viungo katikati ya uwanja.
Aishi Manula, Erasto Nyoni, David Mwantika, kaimu nahodha Aggrey Morris, Himid Mao Mkami, Salum Abubakary, Kipre Tchetche, Kipre Bolou wote hao walianza katika mchezo wa kichapo mwaka jana na wanataraji kuanza katika mchezo wa leo ambao utakuwa watatu mfululizo kwa kikosi chao cha Azam FC katika Ngao ya Jamii. Mabingwa hao wa ligi kuu Bara msimu uliopita, wana safu kabambe ya mashambulizi ambayo ilifunga mabao 12 katika michezo mitano ya Kagame Cup, Mwezi uliopita nchini Rwanda.
Wakati kocha wa Yanga, Maximo akitaraji kumuanzisha mshambulizi mmoja mbele, huku akitegemea safu ya kiungo kama muhimili wa timu, Joseph Omog yeye yupo tofauti , licha ya kumkosa nahodha wake John Bocco, kocha huyo raia wa Cameroon atakuwa na nafasi nzuri ya kujaribu safu yake ya ‘ washambulizi watatu wa kimataifa’. Tchetche, Mhaiti, Lieonel Saint na Mrundi, ‘ Kavu’ ambaye alifunga mabao 22 katika misimu miwili ya ligi kuu Bara akiwa na kikosi cha Yanga. Yanga watapata shinda lakini sehemu yao ya katikati ya uwan ja inatakiwa kuwa ngumu zaidi ya ilivyokuwa katika michezo minne iliyopita ya maandalizi ambayo wameshuhudia timu yao ikifunga mabao matano tu.
AZam ni lazima watafunga, wanaweza kufunga hata mabao mawili kwa sabu safu yao ya mashambulizi ina wafungaji wa uhakika. Kama Leonel ataachana na tabia yake ya kutotoa ushirikiano na kujiona staa zaidi ya wenzake itaendelea Azam itaanguka na wanaweza kupoteza mchezo. Safu ya ulinzi ya Yanga ndiyo ile inayotumika katika timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, golikipa Deogratius Munish ana nafasi kubwa ya kuanza mchezo huo lakini nafasi hiyo inaweza kuangukia kwa ‘ mwalimu wa uwanjani’ Juma Kaseja,  nahodha Nadir, Kelvin a Oscar Joshua katika upande wa kushoto ni nafasi nne ambazo zinapangika kwa urahisi.
Maximo  kama ilivyo kwa Omog naye atakuwa akikuna kichwa, ni mlinzi gani sahihi wa kulia ambaye anatakiwa kumpanga katika mfumo wake na kufanya vizuri. Abdul au Telela? Ogog atakuwa akitafakari nafasi hasa ya kumpanga Nyoni mchezaji ambaye anaingia katika mifumo yote. Nani atamchezesha nafasi ya ulinzi wa kushoto? Ni Nyoni, Said Mourad au kinda Gadiel Michael ambaye alifanya vizuri katika michuano ya Kagame?. Makocha wote wanapasuka vichwa, hiyo ni kutokana na wachezaji wa timu pinzani jinsi wanavyocheza na u-fit wao walionao sasa.
Maximo amekuwa akitumia mfumo wa  4-5-1 ambao huwapanga viungo watano, Hasan Dilunga upande wa kulia,  Mbuyu kama kiungo wa kwanza wa ulinzi-namba 6,  Andrey Coutinho kama kiungo wa mashambulizi akitokea upande wa kushoto, Niyonzima kama kiungo ‘ mchezesha timu mkuu’ –namba 8, Msuva amekuwa akitumika kama mshambulizi wa pili. Kwa nini imekuwa hivyo? Mbuyu ni mkabaji hasa na mchezaji anayeanzisha pasi nzuri kwa viungo wa mbele. Dilunga ni mchezaji mwenye nguvu katika miguu na mwili wake , ni mwepesi hivyom ni rahisi kwake kucheza kama kiungo wa kulia, wakati mwingine upande wa kushoto, kama ataendelea kupiga pasi zinazofika bila shaka ni chaguo ambao Maximo hatajutia. Vipi kuhusu nafasi ya Mrisho Ngassa? Maximo anaweza kumpanga Nassa kama mshambulizi wa pili nyuma ya GEilson Santos ‘ Jaja’ na ikiwa hivyo itamaanisha Dilunga arudi katika benchi na Msuva acheze kama kiungo wa kulia. Itafaa zaidi , Ngassa akicheza, kwa sababu viungo wa Azam ni ‘ wagumu na hawachoki’ mapema. Himid, Salum, na Bolou itakuwa safu nzuri ya kiungo kwa upande wa kikosi cha Omog, lakini anaweza kumtumia Nyoni katika eneo hilo ikiwa atachezesha timu yake katika mfumo wa 4-4-2.
Azam wana safu nzuri ya ulinzi ambayo kwa kiasi kikubwa ilichangia mafanikio ya timu hiyo katika ligi kuu Bara msimu uliopita waliporuhusu mabao 15 katika michezo 26. Morris, Mwantika ni chaguo zuri la kwanza katika safu ya ulinzi wa kati. Jaja atafunga katika mchezo wa leo ikiwa viungo wake watamiliki mchezo. Shomari Kapombe atakutana na kiungo mwenye maarifa, Couinho na upande wa kulia wa Azam umekuwa na mchezo usioridhisha sana kwani upande huo upitika kiurahisi, ili kuziba nafasi ya Yanga kutumia upande wao wa kushoto Omog ni lazima amuanzishe nje mshambulizi wake mmoja ili kumpatia nafasi Nyoni katika eneo la kiungo kuwasaidia, Himid, Salum na Bolou.
Said Mourad atakuwa na nafasi finyu ya kuanza katika safu ya ulinzi wa kati, lakini ili kuleta usawa na nguvu zaidi katika ngome, Omog anaweza kupata faida kubwa akimpanga mchezaji huyo katika eneo la ulinzi wa kushoto.  Ni mechi ngumu lakini inaweza kuwa ya mabao mengi, 3-2, 2-1 au 3-1 ni matokeo ambayo yanaweza kutokea. Ipi timu bora zaidi katika mchezo wa leo? Yanga? Ubora wao uko wapi?
Azam ikiimaliza sehemu ya kiungo ya Yanga watashinda, ila watafungwa wakiruhusu vipaji vya Yanga kutawala katikati ya uwanja. Kavumbagu atafunga, Jaja atafunga ila ningempanga Telela katika eneo la kiungo la Yanga ili kuwamudu Azam FC ‘ mwanzo-mwisho’. Ningempanga Nyoni katika kiungo na Mourad katika safu ya beki tatu ili kupunguza krosi za Yanga. Yanga ina nafasi ya kushinda kwa mara nyingine….AZam FC ililazwa na Simba SC kwa mabao 3-2, 2012, wakapoteza mbele ya Yanga kwa bao 1-0, 2013, 2014 itakuwaje, Ngao ya Jamii si bahati yao?



Bondia Elick Mwenda kushoto wa Malawi akikwepa ngumi  wakati wa mpambano wake na bondia Allybaba Ramadhani   uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Allybaba alishinda kwa pointi mpambano huo 
Bondia Raymond Mbwago kushoto akipambana na Iddi Pialali wakati wa mpambano wao uliofanyika Moshi katika ukumbi wa YMCA Hall Pialali alishinda kwa K,O ya raundi ya Nne
Allybaba Ramadhani
Bondia Raymond Mbwago kushoto akipambana na Iddi Pialali wakati wa mpambano wao uliofanyika Moshi katika ukumbi wa YMCA Hall Pialali alishinda kwa K,O ya raundi ya Nne
Bondia Shomari Milundi kushoto akipambana na Saimoni Zabron wakati wa mpambano wao uliofanyika Moshi mpambano huo walitoka Droo ya kufungana 


Bondia Said Yazidu kushoto akipigwa ngumi na Djamal Dahou wa Algelia Dahou alishinda kwa K,O ya raundi ya kwanza ya mpambano huo



Wachezaji wa Simba na Ndanda FC wakiingia Uwanjani wakati wa mchezo wa maalum wa kusherehekea Ndanda Day uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara na kudhaminiwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), kupitia mpango wake wa Wakulima Scheme. Timu hizo zilitoka suluhu. (Na Mpiga Picha Wetu)

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali mstaafu Joseph Simbakalia akisalimia na timu ya Ndanda FC kabla ya mchezo wao na timu ya Simba uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali mstaafu Joseph Simbakalia akikagua timu ya Simba wakati wa mchezo wa kirafiki na timu ya Ndanda FC uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.

Kikosi kamili cha timu ya Simba kilichopambana na Ndanda FC.
Kikosi cha Ndanda FC kikiwa klatika picha ya pamoja kabla ya pambano lao na Simba.

Wachezazaji wa Simba na Ndanda wakichuana katika uwanja wa Nangwanda Sijaona.

Mashabiki wa soka wakifuatilia pambano la Simba na Danda FC.NSSF kupitia mpango wake wa Wakulima Scheme yadhamini mechi ya kujipima nguvu kati ya Simba ya Dar es Salaam na Ndanda FC ya Mtwara kwenye uwanja wa CCM wa Nangwanda Sijaona na kuhudhuriwa na maelfu ya washabiki wa soka mkoani Mtwara.

Mchezo huo pia ulikuwa ni sehemu ya sherehe za Ndanda Day ulihudhuriwa na viongozi mbali mbali wakiwemo wa Serikali uliisha kwa matokeo ya timu hizo kutoka suluhu.
NSSF kupitia mpango maalum wa wakulima schemes wenye lengo la kuandikisha na kuhudumia wakulima kwenye mfuko ya hifadhi ya jamii nchini ili kuwawezesha wakulima wote nchini wawe kwenye mfuko huo kupata pensheni ya uzeeni pindi watakapo fikisha umri wa miaka 55 na kuendelea wakulima hao wataweza kulipwa penshion zao hadi watakapo fariki.

waliotembelea blog