Sunday, September 14, 2014



Wachezaji wa Simba na Ndanda FC wakiingia Uwanjani wakati wa mchezo wa maalum wa kusherehekea Ndanda Day uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara na kudhaminiwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), kupitia mpango wake wa Wakulima Scheme. Timu hizo zilitoka suluhu. (Na Mpiga Picha Wetu)

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali mstaafu Joseph Simbakalia akisalimia na timu ya Ndanda FC kabla ya mchezo wao na timu ya Simba uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali mstaafu Joseph Simbakalia akikagua timu ya Simba wakati wa mchezo wa kirafiki na timu ya Ndanda FC uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.

Kikosi kamili cha timu ya Simba kilichopambana na Ndanda FC.
Kikosi cha Ndanda FC kikiwa klatika picha ya pamoja kabla ya pambano lao na Simba.

Wachezazaji wa Simba na Ndanda wakichuana katika uwanja wa Nangwanda Sijaona.

Mashabiki wa soka wakifuatilia pambano la Simba na Danda FC.NSSF kupitia mpango wake wa Wakulima Scheme yadhamini mechi ya kujipima nguvu kati ya Simba ya Dar es Salaam na Ndanda FC ya Mtwara kwenye uwanja wa CCM wa Nangwanda Sijaona na kuhudhuriwa na maelfu ya washabiki wa soka mkoani Mtwara.

Mchezo huo pia ulikuwa ni sehemu ya sherehe za Ndanda Day ulihudhuriwa na viongozi mbali mbali wakiwemo wa Serikali uliisha kwa matokeo ya timu hizo kutoka suluhu.
NSSF kupitia mpango maalum wa wakulima schemes wenye lengo la kuandikisha na kuhudumia wakulima kwenye mfuko ya hifadhi ya jamii nchini ili kuwawezesha wakulima wote nchini wawe kwenye mfuko huo kupata pensheni ya uzeeni pindi watakapo fikisha umri wa miaka 55 na kuendelea wakulima hao wataweza kulipwa penshion zao hadi watakapo fariki.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog