Monday, December 22, 2014


MCHEZAJI BORA DUNIANI Cristiano Ronaldo amerudi kwao huko Mji wa Funchat kwenye Kisiwa cha Himaya ya Ureno cha Madeira hii Leo Jumapili kuhudhuria uzinduzi maalum wa Sanamu yake ya kumuenzi kwa mafanikio yake.
Mara baada ya Jana kuisaidia Klabu yake Real Madrid kutwaa Kombe la Dunia kwa Klabu baada ya kuichapa San Lorenzo ya Argentina Bao 2-0 huko Marrakech, Nchini Morocco, Ronaldo aliruka moja kwa moja kwenda Madeira.

Akiongea kwenye uzinduzi huo wa Sanamu yake huku akizungukwa na Familia yake pamoja na Maelfu ya Mashabiki, Ronaldo, ambae alijawa hisia, alitamka: “Huu ni wakati spesho kwangu, kuweka Sanamu yangu!”
Nae Mama yake Mzazi Ronaldo, Dolores Aveiro, alisema: “Ronaldo hajasahau asili yake.”
Sanamu hiyo yenye Urefu wa Mita 3.4 ni sehemu ya mkusanyiko wa Mataji na Tuzo mbalimbali ambazo Ronaldo amezitwaa katika maisha yake ya Soka na kuhifadhiwa kwenye Makumbusho yake maalum hapo Kisiwani Madeira zikiwemo Ballon d'Or mbili huku akiwekewa matumaini makubwaya kutwa ya tatu ifikapo Januari 12.

RONALDO ATUA KWAO MADEIRA, TAYARI KWA UZINDUZI WA SANAMU YAKE!

MCHEZAJI BORA DUNIANI Cristiano Ronaldo amerudi kwao huko Mji wa Funchat kwenye Kisiwa cha Himaya ya Ureno cha Madeira hii Leo Jumapili kuhudhuria uzinduzi maalum wa Sanamu yake ya kumuenzi kwa mafanikio yake.
Mara baada ya Jana kuisaidia Klabu yake Real Madrid kutwaa Kombe la Dunia kwa Klabu baada ya kuichapa San Lorenzo ya Argentina Bao 2-0 huko Marrakech, Nchini Morocco, Ronaldo aliruka moja kwa moja kwenda Madeira.

Akiongea kwenye uzinduzi huo wa Sanamu yake huku akizungukwa na Familia yake pamoja na Maelfu ya Mashabiki, Ronaldo, ambae alijawa hisia, alitamka: “Huu ni wakati spesho kwangu, kuweka Sanamu yangu!”
Nae Mama yake Mzazi Ronaldo, Dolores Aveiro, alisema: “Ronaldo hajasahau asili yake.”
Sanamu hiyo yenye Urefu wa Mita 3.4 ni sehemu ya mkusanyiko wa Mataji na Tuzo mbalimbali ambazo Ronaldo amezitwaa katika maisha yake ya Soka na kuhifadhiwa kwenye Makumbusho yake maalum hapo Kisiwani Madeira zikiwemo Ballon d'Or mbili huku akiwekewa matumaini makubwaya kutwa ya tatu ifikapo Januari 12.



JANA Usiku huko Marrakech, Nchini Morocco, ndani ya Le Grand Stade de Marrakech
Unaopakia Watu 45240, Mabingwa wa Ulaya Real Madrid wameichapa San Lorenzo ya Argentina Bao 2-0 na kutwaa Kombe la Dunia kwa Klabu.

Hii ni mara ya kwanza kwa Real kutwaa Kombe hili ambalo ni Mashindano ya FIFA ingawa wameshawahi kutwaa Intercontinental Cup mara 3 ambalo lilikuwa likifanana na hili ingawa hilo lilishindaniwa na Mabingwa wa Ulaya dhidi ya Mabingwa wa Marekani ya Kusini tu.

Bao za Real hapo Jana zilifungwa na Sergio Ramos na Gareth Bale huku Mchezaji Bora Duniani, Cristiano Ronaldo, akipata nafasi moja tu ya kufunga ambayo Kipa Torrico aliakoa.

Hivi sasa Real wapo kwenye wimbi la ushindi wa Mechi 22 mfululizo na wanaikimbiza Rekodi ya Dunia ya kushinda Mechi 24 mfululizo inayoshikiliwa na Klabu ya Brazil, Curitiba, waliyoiweka Mwaka 2011.
Real pia wamekamataTaji lao la 4 kwa Mwaka 2014 kitu ambacho walikuwa hawajahi kukifanya baada ya kuwahi kutwaa Mataji Matatu tu ndani ya Mwaka mmoja lakini Mwaka huu 2015 wamefanikiwa kubeba UEFA CHAMPIONS LIGI, Copa del Rey, UEFA SUPER CUP pamoja na Kombe la FIFA la Klabu Bingwa Duniani.

Vile vile wamemaliza Mwaka 2014 kwa kuwa Vinara wa Ligi ya kwao Spain La Liga wakiwa Pointi 1 mbele ya Mahasimu wao FC Barcelona ambao wamecheza Mechi moja zaidi.

Mapema hiyo Jana, kwenye Mechi ya kusaka Mshindi wa 3, Auckland City ya New Zealand iliishinda Cruz Azul kwa Mikwaju ya Penati 4-2 baada ya Sare ya Bao 1-1.
Bao za Real Madrid zilifungwa na Sergio Ramos kipindi cha kwanza dakika ya 37 na bao la pili dakika ya 51 kupitia kwa Gareth Bale katika kipindi cha pili Huko Marrakech, Nchini Morocco, ndani ya Stade de Marrakech.Bale akishangilia bao lake la pili



Jokate na Guoxun wakionyesha mikataba baada ya kusaini

Jokate na Guoxun wakibadilishana mikataba baada ya kusaini.

Jokate Mwegelo akizungumza katika hafla hiyo

Afisa Mtendaji mkuu wa kampuni ya Rainbow Shell Craft Company Limited (CEO), Deng Guoxun akuzungumza katika hafla hiyo

Jokate akiteta jambo na Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa kwenye hafla hiyo

Wageni mbalimbali waalikwa wakishughudia hafla hiyo

Meya wa Manispaa ya Ilala akiteta jambo na Mbunge wa Viti maalum (CCM) Mariam Kisangi katika hafla hiyo.

Dar es Salaam. Mbunifu mavazi, Miss Tanzania wa namba mbili 2006, mwanamuziki na muigizaji wa filamu, Jokate Mwegelo amesaini makubaliano yenye thamani ya Sh8.5 billion na kampuni ya Kichina, Rainbow Shell Craft Company Limited kwa ajili ya kuzalisha na kuuza bidhaa mbalimbali za lebo yake ya Kidoti.Makubaliano hayo yalisainiwa leo kwenye hotel ya Serena baina ya Jokate na Afisa Mtendaji mkuu wa kampuni ya Rainbow Shell Craft Company Limited (CEO), Deng Guoxun.

waliotembelea blog