Friday, June 5, 2015


MAELFU ya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi CCM, na wakazi wengine wa jiji la Mwanza, leo Ijumaa Juni 5, 2015, walifurika kwa wingi kwenye ofisi za CCM wilaya ya Nayamagana na ile ya Ilemela, wengine wakitaka kumuona na kupeana mikono na wengine kwa nia ya kumdhamini Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Edwrad Lowassa, alipofika jijini Mwanza kutafuta wana CCM wa kumdhamini katika safari yake ya Matumaini. (Kuwania urais wa Tanzania kupitia CCM.

Madereva texi, waendesha bodaboda, na hata wafanyakazi na wasafiri kwenye uwanja wa ndege wa Mwanza, waliacha shughuli zao kwa muda ili walau wamuone mtangaza nia huyo wa nafasi ya jurasi kupitia CCM.
Lowassa alichukua fomu, za kuomba kuteuliwa na CCM kuwania urais wa Tanzania, Alhamisi Juni 4, 2015 pale makao makuu ya CCM, na safari yake ya kusaka wadhamini ilianza “chap chap” pale pale Dodoma, na Mwanza ndio kituo cha kwanza nje ya Dodoma, ambacho Lowassa, ameanza kampeni yake ya kusaka wadhamini.
Picha ni, Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, ambaye tayari amechukua fomu za kuomba CCM imteue kuwania urais, Edwrad Lowassa, akipungia mkono maelfu ya wanachama wa chama hicho na wananchi wengine baada ya kupata wadhamini kwenye ofisi ya CCM wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza Ijumaa Juni 5, 2015. (Picha na K-VIS MEDIA)




Lowassa, akipokea fomu za wadhamini ambazo tayari zimejazwa na wana CCM wilaya ya Ilemele, kutoka kwa Katibu wa CCM wilayani humo, , Loti Olele Mtui Lazaro

Mmoja wa madereva Texi, akionyesha bango la kumuunga mkon o Lowassa, katika safari ya matumaini 2015

Lowassa, akipokea fomu zilizojazwa na wadhamini ambao ni wanachama wa CCM, kutoka kwa Katibu wa CCM wilaya ya Nyamagana, mkoani Mwanza, Elias Mpanda

Mwanachama mkongwe wa CCM, Mzee Rutaraka, akitoa salamu zake kwa niaba ya wazee jijini Mwanza

Watoto wa Chipukizi kutoka Chama Cha Mapinduzi, jijini Mwanza, Marie Kighei Joseph, (wapili kulia) na Sarafina Magabe, wakimkabidhi zawadi ya maua ikiwa ni ishara ya kumkaribisha Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Edward Lowasa, alipowasili kwenye uwanja wa ndege wa Mwnza, Ijumaa Juni 5, 2015, ili kuomba wadhamini baada ya kuchukua fomu za kuomba kuwania urais wa Tanzania kuputia CCM

Lowassa, akiteremka kutoka ndani ya ndege baada ya kuwasili jijini Mwanza kuomba wadhamini.

Wananchi waliokuwa na kiu ya kumuona Lowassa, walilazimika kupanda juu ya viti kutokana na msongamano wa watu waliofurika kwenye mitaa jirani na odfisi za CCM wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza Ijumaa Juni 5, 2015.

Wasafiri na wafanyakazi wa uwanja wa ndege wa Mwanza, waliacha shughuli zao ili walau wapate kumuona Lowassa, alipowasili kwenye uwanja wa ndege wa Mwnaza Ijumaa Juni 5, 2015, tayari kutafuta wadhamini.


Lowassa, akionyesha fomu ambayo tayari imejazwa na wadhamini wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza


James Milner wa Man City ajiunga na Liverpool.
Liverpool wameafikiana Dili ya kumsaini Kiungo wa England James Milner ambae anachezea Manchester City kwa Uhamisho wa bure.
Milner, mwenye Miaka 29, ameshakubaliana malupulupu yake binafsi na Liverpool na atajiunga rasmi nao kama Mchezaji Huru wakati Mkataba wake na City utakapomalizika hapo Julai Mosi kama akifuzu upimwaji Afya yake.
Akiwa na City kwa Miaka Mitano, Milner alifanikiwa kutwaa Ubingwa wa Ligi Kuu England mara 2, FA CUP na Kombe la Ligi, Capital One Cup.

Milner pia ameichezea England mara 53.
Msimu uliopita, Milner alianza Mechi 24 na kufunga Bao 8 na kuifungia City Bao 8.
Mchezaji huyu alijiunga na City iliyokuwa chini ya Roberto Mancini Mwaka 2010 kwa Dau la Pauni Milioni 26 akitokea Aston Villa na kuichezea Klabu hiyo jumla ya Mechi 125 na kufunga Bao 18.
Klabu nyingine alizowahi kuzichezea ni Newcastle United na Klabu ya Mji wa Nyumbani kwao Leeds United ambayo alianza kucheza Ligi Kuu England kwa mara ya kwanza Mwaka 2002 akiwa na Miaka 16 tu.

Ilkay Gundogan kujiunga na Manchester United msimu wa 2015/16? Klabu kama Barca, AC Milan na Bayern Munich zilikuwa zikihitaji sahihi yake huku mapema tetesi zikisema wenda akapimwa afya kujiunga na Barcelona.Man United 'set to announce £19.5m transfer, terms already agreed'Ilkay Gundogan Christian Funchs wa Schalke atua Leicester CityMemphis Depay wa PSV - Ni wa Manchester United mpaka sasa akitokea PSV EindhovenMorgan Schneiderlin kujiunga na Klabu ya Man United baada ya kushinda mbio hizo huku Klabu ya Arsenal nayo ikiwa kwenye mchakato huo huo wa kumwania mchezaji huyo.Christian Atsu  wa Chelsea atua kwa Mkopo BournemouthPhilipp - Bayer Leverkusen kwenda Stoke Xavi - Al -SaddKipa Artul Borus - Southampton kwenda BournemouthGraham Dorrans - West Brom kwenda NorwichJoshua King - Blackburn kwenda BournemouthWinger wa Benfica Nicolas Gaitan nae inasemekana kujiunga na Man United
Boyata wa Man City kwenda CelticLuiz Gustavo anukia Old Trafford

waliotembelea blog