Wednesday, January 6, 2016


Baada ya kufukuzwa kazi kwa aliyekuwa kocha wa klabu ya Real Madrid ya Hispania Rafael Benitez, January 6 ndio siku ambayo ameongea kauli yake ya kwanza toka atimuliwe kazi na nafasi yake ichukuliwe na Zinedine Zidane.  Benitez amefunguka na kumshukuru kila mmoja ndani ya Real Madrid.
“Kwa sasa nimeondoka Real Madrid kama kocha, napenda kuaga na kumshukuru kila mmoja ndani ya klabu, nataka kila mmoja ndani ya klabu kuanzia mashabiki, bodi ya uongoz wafahamu kuwa naheshimu na ni heshima kwangu kupewa nafasi ya kuifundisha klabu kama Real Madrid” >>> Benitez
Benite
Kocha huyo ambaye hakufanya vizuri ndani ya Real Madrid, aliwahi kutwaa taji la klabu Bingwa Ulaya mwaka 2005 akiwa na Liverpool, Kombe la Laliga akiwa na Valencia na Kombe la klabu Bingwa dunia akiwa na klabu ya Inter Milan ya Italia.

waliotembelea blog