Friday, July 11, 2014

Bingwa mara tatu Ujerumani na bingwa mara mbili Argentina zitagombania dola milioni 35 kwenye mechi ya fainali ya kombe la dunia Jumapili Julai tarehe 13 mjini Rio De Janeiro.
Shirikisho la kimataifa Fifa limetoa jumla ya dola milioni 576 kushindaniwa kwenye mashindano ya mwaka huu nchini Brazil.
Mshindi ataweka kibindoni dola milioni 35 na wa pili $25 milioni, wa tatu $22milioni wa nne $20 milioni.
Timu nne zilizoondolewa kwenye robo-fainali zitapokea $14 milioni kila mmoja, timu nane zilizong'olewa raundi ya pili $9 milioni na timu 16 zilizoondolewa raundi ya kwanza $8 milioni kila mmoja.
Ujerumani imefuzu kwa fainali baada ya kuiadhibu Brazil mabao 7-1 na Argentina ikaiondoa Uholanzi mabao 4-2 ya penalti mechi ya nusu-fainali. Kwa jumla timu 32 zimeshiriki mashindano ya mwaka huu kwenye mechi 64 na wachezaji 736 wakajitosa uwanjani.
Argentina ilifuzu baada ya kushinda Uholanzi
Miongoni mwa wachezaji nyota kwa upande wa Ujerumani ni mfungaji bora zaidi kwenye mashindano haya Miroslav Klose huku Argentina ikijivunia Lionel Messi mshindi wa tuzo la mchezaji bora duniani mara nne.
Hii ni mara ya tatu Ujerumani na Argentina wanakutana fainali ya kombe la dunia, mara ya kwanza ikiwa mwaka wa 1986 nchini Mexico Argentina ikashinda 3-2 kisha wakapatana tena mwaka wa 1990 nchini Italia na Ujerumani ikalipiza kisasi kwa kuinyoa Argentina bao 1-0.
Wadadisi wengi wa kandanda wanasema Ujerumani wana nafasi nzuri zaidi ya kuibuka mshindi kwani wameonyesha kiwango cha juu zaidi ya Argentina kufikia sasa.
Lakini mpira unadunda hivyo basi Argentina nao pia waeza kuibuka mshindi ikikumbukwa kwamba hamna timu ya bara Ulaya imewahi kunyakua ubingwa wa dunia mashindano haya yakifanyika Marekani Kusini.
Kwa jumla mataifa ya Marekani Kusini yameibuka mshindi mara tisa kwenye kombe la dunia na ya Ulaya mara kumi Italia na Ujerumani wakiongoza kwa kushinda mara tatu kila mmoja na Brazil ikiwa juu Marekani Kusini kwa kushinda mara tano, Argentina na Uruguay mara mbili kila mmoja.
FIFA yakatalia mbali rufaa ya Suarez
Shirikisho la soka Duniani FIFA limekatalia mbali ombi la rufaa la mchezaji wa Uruguay Luis Suarez dhidi ya marufuku yake ya mizi minne kwa kosa la kumng'ata Mlinzi wa Italia .
Katika barua kwa wanahabari FIFA ilisema kuwa imekatialia mbali ombi la Shirikisho la Soka la Uruguay la kuitaka kupunguza adhabu ya Mshambulizi huyo wa Liverpool .
Hata hivyo Suarez anauhuru wa kukata rufaa katika mahakama ya rufaa ya michezo (Court of Arbitration for Sport) iwapo hataridhika na Uamuzi huo.
Mshambulizi huyo wa Liverpool alibanduliwa nje ya kombe la dunia baada ya tukio hilo la Juni tarehe 24 na sasa anaomba msamaha ili iwe rahisi kwake angalau kujifua pamoja na wachezaji wenza huko Anfield Uingereza huku akitarajia uhamisho kuelekea Uhispania katika klabu ya Barcelona .
Papa Francis na Papa Benedict kushabikia fainali ya kombe la dunia ?
Je ushawahi kushabikia smechi ya kandanda baina ya mahasimu wawili wa jadi ?
Sasa hebu fikiria Mashabiki wa mechi ya fainali kuwa ni Viongozi wa kidini .
Taswira hiyo huenda ikakamilika siku ya jumapili Papa Francis ambaye ni Raiya wa Argentina akitizama mechi baina ya Argentina na Ujerumani na Papa mtangulizi wake Benedicto 16 raiya wa Ujerumani.
Makao makuu ya Kanisa Katoliki hata hivyo imekuwa wazi ikisema kuwa hilo huenda lisikamilike kwani papa Benedicto sio shabiki sugu ukimlinganisha na papa Francis ambaye ni shabiki sugu wa Argentina.
Msemaji wa Vatican Federico Lombardi akisema kuwa labda kadinali mkuu wa zamani wa Buenos Aires Jorge Bergoglio yaani papa Franci atatizama fainali hiyo.
Argentina na Ujerumani zilichuana katika fainali ya kombe la dunia 1986
Papa Benedict XVI, 87, anajulikana kuwa msomi na pia mwenye uraidbu wa mziki wa ala mara nyingi akipapasa roho yake kwa kucheza piano .
Wangdani wa Vatican ahata hivyo wanasema kua katika enzi zake Papa Benedict XVI alikuwa hawezi kosa matokeo ya mechi za klabu anayoishabikia ya Bayern Munich.
Gazeti moja la Italia''the Osservatore Romano'' ndilo lililotibua uvumi huu lilipochapisha habari kabla ya kuanza kwa kombe la dunia lilipobashiri kuwa Argentina itakutana na Ujerumani katika fainali ya kombe la dunia na hivyo kushuhudia mashabiki wa haiba yake , papa Benedicto wa 16 na papa Francis .

download (2) 
KATIKA fainali za mwaka 1986, Diego Maradona aliifungia Argentina au kutoa pasi za mwisho katika mabao 10 ya nchi hiyo. Mwaka huu, Messi amefunga au kutoa pasi katika mabao 8 ya Arggentina. Maradon pia alikabiliana na Ujerumani (Ujerumani Magharibi kwa wakati huo) katika mchezo wa fainali, lakini hakufunga goli katika mechi hiyo.

download 
Carlos Queiroz alijiuzulu nafasi yake ya ukocha wa timu ya taifa ya Iran baada ya nchi hiyo kutolewa hatua ya makundi katika fainali za kombe la dunia mwaka huu nchini Brazil.
Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Mtandao 0712461976 HAPA tunaangalia kwanini Asia imeshindwa kufanya vizuri katika fainali za kombe la dunia mwaka huu nchini Brazil.
1.     UKOSEFU WA UONGOZI Wakati kocha wa Korea Hong Myung-bo anasafiri kwenda Uholanzi mwezi machi mwaka huu kumtembelea Park Ji-sung, hakwenda kuangalia wachezaji muhimu bali ni kumshawishi nyota huyo aachane na mpango wa kustaafu soka la kimataifa. “Timu ya vijana inahitaji wakongwe,” alisema Hong. Park alipotezea wazo lile, lakini ni ukweli kuwa Korea ilikosa wachezaji wenye uzoefu na viongozi kama yeye.  Pia  Japan haikuwa na wachezaji ambao wangepewa majukumu ya kuwaongoza vijana uwanjani katika mazingira tofauti tofauti ya mechi.
2.   MAKOSA YA MAKOCHA Alberto Zaccheroni alikuwa na maandalizi kamili yaliyochukua hadi miaka minne tangu alipokabidhiwa timu ya Japan, lakini bado kocha huyo raia wa Italia hajaweza kuonesha kiwango kizuri katika hatua ya makundi. Japan ilicheza mpira wa kawaida dhidi ya Ivory Coast na Ugiriki. Alikosolewa kwa kumuanzisha Yasuhito Endo  dhidi ya Waafrika, pia aliendelea kumuacha Yasuyuki Konno katika idara ya ulinzi wakati alishindwa kufanya kazi yake na angemtumia hata  Zaccheroni kutokana na kiwango chake kuwa kizuri kwa wakati ule.
Kocha wa Korea, Hongg, hakuwa na wachezaji wenye uzoefu, lakini alishindwa kuwatumia vijana wake katika safu ya ulinzi na hakusikiliza ushauri wa vyombo vya habari na mashabiki na kuendelea kumtumia mshambuliaji butu Park Chu-young. Carlos Queiroz alikuwa na kiwango kizuri, labda atajuta baada ya kushindwa kuonesha ubora wake na kuisaidia timu kwenye mechi dhidi ya Bosnia.

article-2688109-1F8DDD0F00000578-722_634x454 
Kwenye rada: Beki wa Atletico Madrid, Javi Manquillo anatakiwa na Arsenal.
KLABU ya Arsenal inafanya jitihada za kumsajili beki wa kulia wa Atletico Madrid , Javi Manquillo.
Washika mtutu hao wa London wanataka kumsajili beki huyo wa Hispania kwa lengo la kuongeza ushindani katika nafasi ya beki wa kulia msimu ujao.
Kama watakamilisha usajili huo, basi Manquillo atachuana katika nafasi hiyo na beki waliomsaini siku chache zilizopita, Mathieu Debuchy.
article-2688109-15AAA01D000005DC-583_634x486 
Njiani kusepa: Carl Jenkinson anaweza kuondoka Asernal na anawindwa zaidi na Newcastle.

article-2688200-1F8E156C00000578-361_634x430 
Hisia: Neymar alimwaga machozi, huku akiweka wazi kuwa alikaribia kuwa kichaa baada ya Juan Zuniga kumfanyia faulo mbaya kwenye mchezo wa robo fainali ya kombe la dunia dhidi ya Colombia.
NYOTA wa Brazil, Neymar Jr amefichua siri kuwa alishindwa kuzuia machozi na alikaribia kuwa kichaa baada ya kugongwa na Juan Zuniga na kuvunjika mfupa wa uti wa mgongo.
Neymar kwa mara ya kwanza alifanya mkutano na waandishi wa habari baada ya kutoka Hospitalini ambapo anauguza majeraha yake ya mfupa wa uti wa mgongo uliovunjika kwenye mechi ya robo fainali ya kombe la dunia dhidi ya Colombia.
article-2688200-1F8E0D0A00000578-115_634x432 
Machozi: Neymar alishindwa kuendelea kucheza fainali za kombe la dunia baada ya kuvunjika mfupa wa uti wa mgongo.
Pia Neymar hajakubaliana na maneno ya wakala wake aliyemuita Luiz Felipe Scolari kuwa ni kocha mbaya, mwenye majivuno na aliyepitwa na wakati.

article-2687497-1F8DF1E800000578-750_634x446Usajili mzuri: Kuna imani kuwa Asernal wanaweza kufanya makubwa msimu ujao baada ya kumsajili  Sanchez.
article-2687497-1F8DF0E800000578-607_634x430Maisha mapya: Alexis Sanchez akipozi katika picha akivalia jezi yake ya Asernal kama ishara ya kufungua ukurasa mpya wa maisha ya soka. 
ARSENAL imekamilisha usajili wa mshambuliaji wa Barcelona, Alexis Sanchez – kwa dau la paundi milioni 30.
Kwa usajili huo, Asernal wanaamini nyota huyo ataweza kuwasaidia katika harakati zao za kutafuta ubingwa wa ligi kuu msimu ujao pamoja na michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya.
Nyota huyo wa Chile ambaye alikatisha likizo yake na kwenda London kukamilisha usajili, alifuzu vipimo vya afya na kukubali kusaini mkataba wa miaka minne-huku kukiwa na kipengele cha kuongeza miezi 12 na mshahara utakuwa paundi laki moja na elfu 40 kwa wiki.

article-2686527-1F849DEE00000578-789_634x510Tabasamu kubwa: Mshambuliaji wa Man City ambaye hajatulia , Alvaro Negredo akicheka wakati alipokuwa anapenda ndege kwenda Dundee.
KIKOSI cha mabingwa wa England, Manchester City kimekwea pipa kwenda Dundee tayari kuanza ziara yao ya maandalizi ya msimu huko Scottish.
Katika msafara huo, pia umemjumuisha mshamabiliaji ambaye hajatulia kwa sasa, Alvaro Negredo aliyeonekana kuwa katika morali nzuri.
Kikosi cha Manuel Pellegrini kitacheza Dundee siku ya jumapili kabla ya kusafiri siku inayofuata kwenda Edinburgh kucheza dhidi ya Hearts siku ya ijumaa.
Negredo anayehusishwa kuondoka Etihad, alipigwa picha akipanda ndege binafsi ya Man City, `City Jet` jana jioni, huku naye kipa mpya, Willy Caballero akiwemo katika msafara huo.
article-2686527-1F849ED200000578-120_634x537Kifaa kipya: Kipa mpya wa Man city, Willy Caballaro pia yumo katika msafara wa klabu hiyo kwenda nchini Scotland kufanya maandalizi ya kabla ya msimu.

article-2687391-02320B6B000005DC-997_634x443 
Gwiji: Mourinho (kushoto alimleta Drogba katika klabu ya Chelsea mwaka 2004 akitokea Marseille ya Ufaransa.
KLABU ya Chelsea inaangalia uwezekano wa kumrudisha Didier Drogba katika dimba la Stamford Bridge.
Nyota huyo mwenye miaka 36 anazivutia klabu za Qatar, wakati Juventus nao wakifikiria kumnasa mkongwe huyo anayecheza katika klabu ya Galatasaray ya Uturuki.
Bado Jose Mourinho ana mahusiano mazuri na Muivory coast huyo na anavutiwa kumrudisha kwa majukumu ya ukocha zaidi.
article-2687391-1C65936400000578-371_634x507 
Mkongwe huyu wa miaka 36 anazivutia klabu za Qatar, nao Juventus wanaitaka saini yake.
Klabu hizo za Qatar zinatarajia kutoa ofa nono na mshahara utajadiliwa, lakini unakadiriwa kuwa paundi milioni 3 kwa msimu baada ya makato ya kodi.
Wazo la kurudi Chelsea litaangaliwa zaidi na pande zote.

waliotembelea blog