Friday, July 11, 2014


article-2687391-02320B6B000005DC-997_634x443 
Gwiji: Mourinho (kushoto alimleta Drogba katika klabu ya Chelsea mwaka 2004 akitokea Marseille ya Ufaransa.
KLABU ya Chelsea inaangalia uwezekano wa kumrudisha Didier Drogba katika dimba la Stamford Bridge.
Nyota huyo mwenye miaka 36 anazivutia klabu za Qatar, wakati Juventus nao wakifikiria kumnasa mkongwe huyo anayecheza katika klabu ya Galatasaray ya Uturuki.
Bado Jose Mourinho ana mahusiano mazuri na Muivory coast huyo na anavutiwa kumrudisha kwa majukumu ya ukocha zaidi.
article-2687391-1C65936400000578-371_634x507 
Mkongwe huyu wa miaka 36 anazivutia klabu za Qatar, nao Juventus wanaitaka saini yake.
Klabu hizo za Qatar zinatarajia kutoa ofa nono na mshahara utajadiliwa, lakini unakadiriwa kuwa paundi milioni 3 kwa msimu baada ya makato ya kodi.
Wazo la kurudi Chelsea litaangaliwa zaidi na pande zote.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog