Friday, July 11, 2014

article-2688200-1F8E156C00000578-361_634x430 
Hisia: Neymar alimwaga machozi, huku akiweka wazi kuwa alikaribia kuwa kichaa baada ya Juan Zuniga kumfanyia faulo mbaya kwenye mchezo wa robo fainali ya kombe la dunia dhidi ya Colombia.
NYOTA wa Brazil, Neymar Jr amefichua siri kuwa alishindwa kuzuia machozi na alikaribia kuwa kichaa baada ya kugongwa na Juan Zuniga na kuvunjika mfupa wa uti wa mgongo.
Neymar kwa mara ya kwanza alifanya mkutano na waandishi wa habari baada ya kutoka Hospitalini ambapo anauguza majeraha yake ya mfupa wa uti wa mgongo uliovunjika kwenye mechi ya robo fainali ya kombe la dunia dhidi ya Colombia.
article-2688200-1F8E0D0A00000578-115_634x432 
Machozi: Neymar alishindwa kuendelea kucheza fainali za kombe la dunia baada ya kuvunjika mfupa wa uti wa mgongo.
Pia Neymar hajakubaliana na maneno ya wakala wake aliyemuita Luiz Felipe Scolari kuwa ni kocha mbaya, mwenye majivuno na aliyepitwa na wakati.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog