Friday, July 11, 2014

download 
Carlos Queiroz alijiuzulu nafasi yake ya ukocha wa timu ya taifa ya Iran baada ya nchi hiyo kutolewa hatua ya makundi katika fainali za kombe la dunia mwaka huu nchini Brazil.
Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Mtandao 0712461976 HAPA tunaangalia kwanini Asia imeshindwa kufanya vizuri katika fainali za kombe la dunia mwaka huu nchini Brazil.
1.     UKOSEFU WA UONGOZI Wakati kocha wa Korea Hong Myung-bo anasafiri kwenda Uholanzi mwezi machi mwaka huu kumtembelea Park Ji-sung, hakwenda kuangalia wachezaji muhimu bali ni kumshawishi nyota huyo aachane na mpango wa kustaafu soka la kimataifa. “Timu ya vijana inahitaji wakongwe,” alisema Hong. Park alipotezea wazo lile, lakini ni ukweli kuwa Korea ilikosa wachezaji wenye uzoefu na viongozi kama yeye.  Pia  Japan haikuwa na wachezaji ambao wangepewa majukumu ya kuwaongoza vijana uwanjani katika mazingira tofauti tofauti ya mechi.
2.   MAKOSA YA MAKOCHA Alberto Zaccheroni alikuwa na maandalizi kamili yaliyochukua hadi miaka minne tangu alipokabidhiwa timu ya Japan, lakini bado kocha huyo raia wa Italia hajaweza kuonesha kiwango kizuri katika hatua ya makundi. Japan ilicheza mpira wa kawaida dhidi ya Ivory Coast na Ugiriki. Alikosolewa kwa kumuanzisha Yasuhito Endo  dhidi ya Waafrika, pia aliendelea kumuacha Yasuyuki Konno katika idara ya ulinzi wakati alishindwa kufanya kazi yake na angemtumia hata  Zaccheroni kutokana na kiwango chake kuwa kizuri kwa wakati ule.
Kocha wa Korea, Hongg, hakuwa na wachezaji wenye uzoefu, lakini alishindwa kuwatumia vijana wake katika safu ya ulinzi na hakusikiliza ushauri wa vyombo vya habari na mashabiki na kuendelea kumtumia mshambuliaji butu Park Chu-young. Carlos Queiroz alikuwa na kiwango kizuri, labda atajuta baada ya kushindwa kuonesha ubora wake na kuisaidia timu kwenye mechi dhidi ya Bosnia.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog