Monday, March 16, 2015

DSC08607NA Mwandishi Wetu,TANGA.
TIMU ya Coastal Union imewasili jijini Tanga ikiwa na mikakati mizito ya kuhakikisha inawanyamazisha wapinzani wao Azam FC ikiwa ni muendelezo wa Michuano ya Ligi kuu soka Tanzania bara mchezo unaotarajiwa kucheza kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani wikiendi ijayo.
Akizungumza leo na waandishi wa habari, Ofisa Habari wa Coastal Union,Oscar Assenga amesema kuwa sasa nguvu zao watazielekeza kwenye mchezo huo utakaochezwa kwenye mjini hapa.
Amesema kuwa dhamira yake aliyoipanga ni kuchukua pointi tatu muhimu dhidi ya Ruvu Shooting haikuweza kutimia na kujikuta wakilazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 hivyo atahakikisha inatimia kwenye mechi hiyo. 
Amesema timu hiyo imerudi salama mkoani hapa na tayari wameshaanza kujipanga imara kuhakikisha mechi hiyo timu inapata ushindi n kutokana na uimara wa kikosi chao
Aidha amesema kuwa wachezaji wa kikosi hicho wameimarika zaidi na wapo imara kuweza kupambana kufa na kupona ili kuchukua pointi tatu muhimuzo zitawasogeza kwenye nafasi za juu kwenye msimamo wa Ligi hiyo.
Hata hiyo amewataka wapenzi na mashabiki wa soka mkoani hapa kuhakikisha wanajitokeza kwa wingi katika mchezo huo ili kuipa hamasa timu hiyo kuweza kutimiza ndoto zake.
Mwisho.


Rooney akishangilia kwa Mashabiki Old Trafford baada ya kuifungia bao la tatu Man United mbele ya Mashabiki 75,112.Boxing!!Rooney akishangilia kwa aina yake baada ya kuifungia bao la mwisho Man United leo dhidi ya SpursDakika ya 34 Kepteni Wayne Rooney alipiga Bao la 3 alipounasa Mpira karibu ya Mstari wa Kati na kuwapita Mabeki wa Spurs Dier na Rose na kisha kumhadaa Kipa Hugo Lloris na kufunga.Mara baada Mpira kutinga wavuni, Rooney alishangilia kwa kucheza Ngumi na kisha kujidondosha chini akivunga amepigwa Ngumi na kuzirai ikiwa ni jibu la habari zilizozagaa mitandaoni hii Leo kuwa alipigwa Ngumi na kuzirai Jikoni Nyumbani kwake wakati akifanya mzaha wa kucheza Ngumi na Mchezaji wa zamani wa Man United Phil Bardsley ambae sasa anacheza Stoke City.Rooney chini akipongezwa na Ashley Young3-03-0 Rooney dakika ya 34 anakatiza kwenye ngome ya Tottennham na kufunga bao la tatu dhidi ya Spurs ambao mpaka kipindi cha kwanza kinamalizika hawakuwa na kitu.Wayne Rooney scores the third goal for Manchester UnitedJuan Mata is challenged by Danny RoseJuan Mata akichuana Marouane Fellaini akipongezwa na MataUnited wakiendesha! Michael Carrick akiwaongoza baada ya kufunga bao la pili kushangilia.2-0Dakika ya 19 Michael Carrick aliwachapa bao la kichwa Spurs na kufanya 2-0. Marouane Fellaini dakika ya 9 aliipachikia bao la kwanza man United na kufanya 1-0 dhidi ya Spurs.Fellaini akishangilia baada ya kufunga bao la kwanzaHarry Kane hakuonekana leo..kafunikwa Old TraffordVIKOSI:
Manchester United XI:
De Gea, Valencia, Jones, Smalling, Blind, Carrick, Herrera, Mata, Fellaini, Young, Rooney.
Tottenham XI: Lloris, Walker, Dier, Vertonghen, Rose, Bentaleb, Mason, Chadli, Eriksen, Townsend, Kane


Baadhi ya Wachezaji wa Chelsea akiwemo Terry wakiwa vichwa chini baada ya kugawana pointi na Sant'sMpaka dakika zinayoyoma ilikuwa ni 1-1John Terry akiwa hoi!!Dakika ya 19 Southampton walisawazisha bao kwa penati kupitia kwa Mchezaji wao Dusan Tadic na kufanya 1-1. 1-1Dusan Tadic hakufanya makosa!Kipindi cha pili pamoja na kwamba kilikuwa cha kushambuliana hakuna aliyeliona lango la Mwenzake. Chelsea wakiwakosa kosa mara kadhaa Saint's.John Terry hapa alikosa bao wazi..Hapa ni England Diego Costa!!Chelsea Chupuchupu wapate bao hapa...mpira uligonga nguzoKashikashi ilitokea ndani ya eneo hatari la penati na Southampton mchezaji wake kuangusha na hatimae kupata penati na  kusawazisha kwa mkwaju huo wa penati kupitia kwa Dusan Tadic.Kipindi cha kwanza dakika 11 Diego Costa aliipatia bao kwa kichwa Chelsea na kufanya 1-0 dhidi ya Southampton.


Wenyeji Everton waliichapa Newcastle Bao 3-0 kwa Bao za Dakika ya 20 za John McCarthy, Penati ya Romelu Lukaku ya Dakika ya 56 na la 3 kwenye Dakika za Majeruhi kupitia Ross Barkley.
Newcastle walimaliza Mechi hii wakiwa Mtu 10 baada ya Beki wao Fabricio Coloccini kupewa Kadi Nyekundu katika Dakika ya 59.

Dakika ya 90 Ross Barkley aliwafungia bao la tatu na la mwisho likihitimisha bao kuwa 3-0 dhidi ya Newcastle na Mtanange kumalizika Everton wakiibuka kidedea.
Kipindi cha pili dakika ya 56 Romelu Lukaku aliwafungia bao la pili kwa mkwaju wa penati na kufanya bao kuwa 2-0 dhidi ya Newcastle United.
J. McCarthy dakika ya 20 kipindi cha kwanza anaipatia bao Everton. Ndani ya Goodison Park raha tupu!!

waliotembelea blog