Monday, September 8, 2014


Maisha yamebadilika: Kiungo Cesc Fabregas alijiunga na Chelsea akitokea Barcelona 

CESC Fabregas amekiri kuwa bado anajihisi kama mchezaji wa Arsenal-licha ya kujiunga na wapinzani wao wa London, klabu ya Chelsea kwa paundi milioni 30 majira ya kiangazi mwaka huu.
Kiungo huyo mshambuliaji wa Hispania tayari ameshaonesha makeke Stamford Bridge kwa kutoa pasi za mwisho nne kwa wachezaji wenzake msimu huu.
Baada ya kuondoka katika klabu yake aliyokulia ya Barcelona-Fabregas anatarajia kurudi katika klabu yake ya zamani ya London Kaskazini akiwa na mkanda mpya wa Chelsea.
Enzi zake: Fabregas, ambaye aliichezea Arsenal kwa miaka 8, amesema siku zote anajihisi kama mchezaji wa Gunners


Furaha: Kiungo wa Hispania,  Fabregas (kushoto)  akishangilia bao la Chelsea dhidi ya Everton mapema msimu huu.
"Kwa wakati wote nitajihisi kama mtu wa Gunners na najua narudi pale (uwanja wa Emirates) na nahisi utakuwa wakati maalumu, lakini nimejifunga na Chelsea," Fabregas aliwaambia El Pais.
"Kumbuka nilicheza fainali ya ligi ya mabingwa dhidi ya Barcelona! naapa kwamba nilifanya kila kitu kuhakikisha tunashinda mechi ile hata kama nilikuwa Barcelona tangu utotoni"


Down and out: Reus looks distraught after going down in the closing stages against Scotland on Sunday
Nje: Reus akiugulia maamuzi katika  mechi ya jana usiku dhidi ya Scotland 

NYOTA wa Borussia Dortmund, Marco Reus ataikosa mechi ya ligi ya mabingwa barani Ulaya dhidi ya Arsenal huko Westfalenstadion kufuatia kuvunjika mfupa wa kifundo cha mguu katika mechi ya kuwania kufuzu fainali za Euro 2016 dhidi ya Scotland.
Mkali huyo wa Ujerumani atakaa nje ya uwanja kwa wiki nne baada ya kukatwa buti na Charlie Mulgrew jana usiku.
Arsenal watasafiri kwenda Ujerumani Septemba 16 mwaka huu kukabiliana na Dortmund katika mechi ya makundi ya ligi ya mabingwa-kwa mara ya nne ndani ya miaka minne ambapo klabu hizo zinapangwa kundi moja na Reus atarudi uwanjani mpaka mapema mwezi oktoba.
Late injury: The Germany winger goes down clutching his left ankle after a Charlie Mulgrew challenge
Balaa gani?: Winga wa Ujerumani akianguka chini baada ya kukatwa buti na Charlie Mulgrew na kuumia kifundo cha mguu wa kushoto
Absent: Reus' club Borussia Dortmund broke the news of his injury on Twitter
Atakosekana: Klabu ya Reus ya Borussia Dortmund ilitangaza taarifa hizo katika mtandao wa Twita.



Wasaniii walioshiriki tamasha la Fiesta 2014 wakiwa na mishumaa jukwaani wakisambaza upendo na kuwafariji wale wote waliopotelewa na ndugu zao,waliojeruhiwa katika ajali iliyotokea hivi karibuni wilayani Butiama mkoani Mara,ambapo watu zaidi ya 40 walipoteza maisha na wengine kujeruhiwa vibaya.

Sehemu ya umati wa wakazi wa mji wa musoma wakiwa ndani ya uwanja wa Karume,wakati tamasha la Fiesta 2014,likiendelea huku shangwe za hapa na pale zikiwa zimetawala kila kona ya uwanja.

Mmoja wa wasanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya,Barnaba ambaye kwa sasa anatamba na wimbo wake mpya ujulikanao kwa jina la Waharade akiwaimbisha wakazi wa mji wa musoma waliojitokeza kwa wingi kwenye tamasha la fiesta 2014

Mmoja wa wasanii kutoka kundi la Weusi ,Nick wa Pili akiwarusha wakazi wa mji wa Musoma usiku huu kwenye tamasha la Fiesta 2014,lililofanyika ndani ya uwanja wa Karume.

Sehemu ya wakazi wa Musoma waliojitokeza kwenye tamasha la Fiesta usiku huu ndani ya uwanja wa Karume.

Mwanadada machachari awapo jukwaani,Shilole akiimba kwa madaha kabisa kwenye jukwaa la Fiesta ndani ya uwanja wa Karume mjini Musoma.

Pichani kati ni msanii wa muziki wa kizazi kipya Rachael akiwa sambamba na madansa wake wakilishambulia jukwaa la fiesta vilivyo usiku huu ndani ya uwanja wa Karume mjini Musoma

Mashabiki wakishangilia burudani iliyokuwa ikitolewa na wasanii mbalimbali jukwaani usiku huu

Mmoja wa wasanii anaeokuja juu katika anga ya muziki wa hip hop,Young Killer a.k.a Msodoki akiimba jukwaani.

Wakazi wa Musoma walivyojitokeza kwenye tamasha la Fiesta 2014 katika uwanja wa Karume usiku huu.

waliotembelea blog