Monday, September 8, 2014


Maisha yamebadilika: Kiungo Cesc Fabregas alijiunga na Chelsea akitokea Barcelona 

CESC Fabregas amekiri kuwa bado anajihisi kama mchezaji wa Arsenal-licha ya kujiunga na wapinzani wao wa London, klabu ya Chelsea kwa paundi milioni 30 majira ya kiangazi mwaka huu.
Kiungo huyo mshambuliaji wa Hispania tayari ameshaonesha makeke Stamford Bridge kwa kutoa pasi za mwisho nne kwa wachezaji wenzake msimu huu.
Baada ya kuondoka katika klabu yake aliyokulia ya Barcelona-Fabregas anatarajia kurudi katika klabu yake ya zamani ya London Kaskazini akiwa na mkanda mpya wa Chelsea.
Enzi zake: Fabregas, ambaye aliichezea Arsenal kwa miaka 8, amesema siku zote anajihisi kama mchezaji wa Gunners


Furaha: Kiungo wa Hispania,  Fabregas (kushoto)  akishangilia bao la Chelsea dhidi ya Everton mapema msimu huu.
"Kwa wakati wote nitajihisi kama mtu wa Gunners na najua narudi pale (uwanja wa Emirates) na nahisi utakuwa wakati maalumu, lakini nimejifunga na Chelsea," Fabregas aliwaambia El Pais.
"Kumbuka nilicheza fainali ya ligi ya mabingwa dhidi ya Barcelona! naapa kwamba nilifanya kila kitu kuhakikisha tunashinda mechi ile hata kama nilikuwa Barcelona tangu utotoni"

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog