Monday, June 29, 2015



xxx 
Baadhi ya Wanamichezo wa Polisi walioshiriki Michezo ya Wakuu wa Majeshi ya Polisi kusini mwa Afrika mwaka 2013 nchini Namibia wakiwa katika picha.

Timu za Jeshi la Polisi Tanzania zitakazoshiriki michezo ya Umoja wa Wakuu wa Majeshi ya Polisi kwa nchi za kusini mwa Afrika (SARPCCO),  mwishoni mwa mwezi julai nchini Swaziland zinaendelea kujifua vyema katika  kambi yao inayoendelea katika chuo cha Taaluma ya  Polisi Dar es Salaam (DPA).
Akizungumza na blog  hii Mkuu wa kitengo cha  michezo cha Jeshi la Polisi, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi SSP Jonas Mahanga alizitaja timu zilizopo kambini kuwa ni  pamoja na Timu ya Mpira wa miguu, pete, riadha na vishale ambapo hivi sasa zinajifua kuhakikisha kuwa zinakuwa vizuri pindi michuano hiyo itakapoanza kutimua vumbi.
Amesema timu hizo zitaanza kucheza michezo ya kirafiki ili kujipima nguvu na kuhakikisha wanafanya vizuri kwa kuwa michezo ya mwaka huu itakuwa na ushindani mkubwa kutokana na nchi zilizothibitisha kushiriki kujipanga vizuri.
SSP Mahanga amesema mpaka sasa nchi kumi na nne zimeshathibitisha kushiriki michuano hiyo na wanaendelea kuwakaribisha wadhamini mbalimbali watakaoweza kusaidia safari hiyo ili kuliletea taifa sifa.
Aidha amesema wachezaji wengi wa riaha wanaendelea na mazoezi katika timu ya taifa ya riadha na wengine wapo nchini Kenya ambapo muda utakapowadia wataungana na wenzao katika kambi hiyo ya Dar es Salaam.
Kwa upande wake kocha  wa timu ya mpira wa miguu Corporal John Tamba amesema wachezaji wake wamekuwa wakionyesha kiwango kizuri katika mazoezi kwa kuwa wengi wao wametoka katika mashindano hivi karibuni.
Amesema wachezaji wengi waliopo kambini wanatoka katika timu za Polisi Morogoro, Dodoma, Dar es Salaam, Tabora na Mara ambapo alisema kupitia michezo ya kirafiki atahakikisha timu yake inakuja na ushindi.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog