Thursday, September 10, 2015



Matarajio yalikuwa ni kwamba Steven Gerrard atarejea Liverpool kwa mkopo Mei, mwakani.


Lakini inaonekana hilo halitakuwepo na kiungo huyo nyota wa zamani wa Liverpool, mwenye miaka 35 sasa, ataendelea kubaki na klabu yake mpya ya LA Galaxy.

Kawaida wachezaji wengi wanaokwenda kucheza Marekani wamekuwa wakirejea England kwa mkopo.

Lakini Kamishna wa Ligi Kuu Marekani (MLS), Don Garber amesema haoni kama kuna sababu ya Gerrard kurudi Liverpool.


Tena akaongeza kwamba wachezaji kuondoka MLS kumekuwa kukiishusha hadhi akitolea mfano wa David Beckham alivyoondoka LA Galaxy na kwenda AC Mnilan.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog