Monday, January 9, 2017


DROO YA RAUNDI YA 4 ya EMIRATES FA CUP imefanyika Leo Usiku huko BT Tower Mjini London ikiendeshwa na Wachezaji wa zamani wa Kimataifa wa England Michael Owen na Martin Keown na Mabingwa Watetezi Manchester United kupangwa kucheza kwao Old Trafford na Wigan Athletics.

Man City na Arsenal zote zimepangwa kucheza Ugenini kwa Arsenal kuivaa Southampton au Norwich na Man City kucheza na Mshindi kati ya Crystal Palace na Bolton.
Liverpool, kama wataifunga Plymouth katika Mechi yao ya Marudiano baada ya Sare, watakuwa kwao Anfield kucheza na Wolves.
Vinara wa Ligi Kuu England, Chelsea, wao wako kwao Stamford Bridge kuivaa Brentford.
Mabingwa Watetezi wa Ligi Kuu England, Leicester City, watacheza Ugenini na Derby County wakati Tottenham wakicheza Nyumbani White Hart Lane na Wycombe.
Mechi 16 za Raundi ya 4 zitachezwa Wikiendi ya Januari 28 na 29.
DROO KAMILI TIMU 16:
Crystal Palace au Bolton v Manchester City
Middlesbrough v Accrington Stanley
Fulham v Hull City
Blackburn v Barnsley au Blackpool
Burnley au Sunderland v Fleetwood au Bristol City
Rochdale v Huddersfield Town
Millwall v Watford
Manchester United v Wigan Athletic
Chelsea v Brentford
Lincoln au Ipswich v Brighton
Southampton au Norwich v Arsenal
Plymouth au Liverpool v Wolves
AFC Wimbledon au Sutton v Cambridge au Leeds
Oxford United v Newcastle au Birmingham
Derby County v Leicester City
Tottenham v Wycombe

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog