Tuesday, June 3, 2014

Fainali za Kombe la Dunia ni uwanja mpana. Ni mahali ambapo vipaji na vipaji vya wanasoka duniani huonekana. Madalali wa kuvumbua na kununua wachezaji [scouts] hufurika kwenye mashindano kama haya wakijua wazi kabisa kwamba pale ndipo watakapoona “lulu” kwa ajili ya vilabu vyao. Kwa maana hiyo kuna kila aina ya harakati za kimichezo na kuonyesha na kuonyeshana vipaji. Hii sio kumaanisha kwamba wachezaji wote mahiri hapa duniani walicheza katika fainali za Kombe la Dunia.La. Wapo wasakata kabumbu kadhaa ambao hawakuwahi kugusa fainali hizi.Mfano ni George Opong Weah na watu kama kina George West nk.

Lakini wakati wengine wakionyesha vipaji ili wang’amuliwe na kubadilisha maisha yao ya kisoka,wapo wale ambao wanashuka dimbani tayari wakiwa na majina [superstars] na ambao dunia tayari inakuwa ikiwaangalia kwa makini kutaka kujua na kuona kile watakachokifanya. Kila timu huwa na mchezaji ambaye hutizamwa zaidi. Kwa umombo unaweza kumuita Key Player. Kila timu,kwa kupenda au kutopenda,huwa ina star player. Hii haimanishi kwamba katika timu hakuna wachezaji wengine wenye majina au wanaoweza pia kuwa stars.La. Ni sheria ya mmoja mmoja inayozingatiwa hapa.

Kwa mujibu wa wataalamu mbalimbali wa soka,wachezaji hawa 32 [mmoja kutoka katika kila timu inayoshiriki fainali za Kombe la Dunia mwaka huu] ndio watarajiwa kuchomoza zaidi huko Brazil. Mpangilio huu hapa ni kutokana na makundi ya FIFA World Cup 2014. NB: Orodha hii inaweza kubadilika kwani imeandikwa kabla timu zote hazijathibitisha wachezaji wake 23 iliyowachagua mwisho. Wengine wanaweza kuumia katika siku hizi za mwisho na hivyo kutokwenda Brazil.Zingatia.
Neymar-Brazil.
Hakuna ubishi kwamba Neymar anayechezea soka la kulipwa Barcelona nchini Spain ndio gumzo kubwa kwa timu ya Brazil. Anatarajiwa kuongoza mashambulizi ya The Kings Of Samba[Brazil]
Oribe Peralta-Mexico
Ingawa wachezaji wengine wa Mexico kama Chicharito na Giovani dos Santos wanatajwa kama ma-star,Oribe Peralta ambaye anacheza katika ligi ya nyumbani katika club ya Santos Laguna, ndiye anaaminika hivi sasa kuwa star zaidi
Luka Modric-Croatia
Hakuna shaka kwamba Luka Modric ndiye mchezaji star zaidi hivi sasa katika timu ya Croatia. Kiungo huyu ambaye hivi sasa anachezea timu ya Real Madrid nchini Spain ameonekana wazi kuwa tegemeo sio tu katika club bali nchi yake Croatia.

Charles Itandje-Cameroon
Ingawa ungetegemea mchezaji kama Samuel E’too kuendelea kuwa star na tegemeo zaidi katika timu ya Cameroon, golikipa Charles Itandje ndio tegemeo na ambaye wengi watapenda kumuona akiokoa mikwaji. Charles ambaye anachezea timu ya Konyaspor nchini Uturuki[kwa mkopo kutoka PAOK FC ya Ugiriki] aling’ara vilivyo katika mchezo dhidi ya Tunisia wakati wa kuwania nafasi ya kwenda Brazil.Google utaona alichofanya.
Diego Costa-Spain
Ingawa bado kuna utata kuhusu hali yake na kama atakuwa fit kabla ya kuanza kwa fainali za Kombe la Dunia huko Brazil,Diego Costa mshambuliaji mahiri wa timu ya Atletico Madrid anatarajiwa kuwa nyota wa Spain. Lakini pia huenda akawa ndiye mchezaji atakayezomewa zaidi huko Brazil kwani Diego ni mzaliwa wa Brazil na angeweza kabisa kuchezea Brazil mwaka huu kama asingeamua kuchezea Spain[pia ni raia wa Spain].Wabrazil hawajaipenda hiyo.
Arjen Robben-Holland[The Netherlands]
Robben,mshambuliaji mahiri ambaye hivi sasa anaendelea kuwika na timu ya Bayern Munich nchini Ujerumani,ndiye mchezaji ambaye ni star zaidi na ambaye ameonyesha kuwa na kile kiwango kinachoitwa “cha dunia”. Ana miaka 30 hivi sasa.
HABARI ZAIDI BOFYA LINK HIYO HAPO

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog