Monday, October 20, 2014


Dakika ya 87 Daley Blind aliisawazishia bao Man United na kufanya 2-2 na kuwaokoa Man United huko Hawthorns kwa sare hiyo ambayo aikuleta mabadiliko kwa timu zote mbili licha ya kugawana pointi moja. Sare hii inambakisha Man United nafasi ya 6 na pointi zake 12 huku West Brom Albion wakibaki nafasi ya 15 na pointi zao 9. Dakika ya 66 kipindi cha pili Saido Berahino aliwachomoka mabeki wa United na kuwafunga bao la pili na kufanya 2-1 dhidi ya United baada ya kutanguliziwa pasi na Chris Brunt.Kipindi cha pili dakika ya 48 Marouane Fellaini aliwasawazishia bao safi Man United baada ya kupata krosi kutoka kwa Di Maria na Fellaini aliingia ndani ya Dimba akitokea benchi kuchukua nafasi ya Ander Herrera katika kipindi cha pili dakika ya 46.Fellaini akishangilia bao lakeStéphane Sessegnon akiruka juu kwa kushangilia baada ya kufunga bao la mapema dakika ya nane. Mpaka dakiks 45 zinakatika za kipindi cha kwanza West Brom Albion ndio walikuwa wanaongoza kwa bao 1-0 dhidi ya Manchester United.Stéphane Sessegnon  akishangilia bao lake mapema kipindi cha kwanza baada ya kuweka 1-0 dhidi ya Man United.Dakika ya 8 kipindi cha kwanza West Brom wanafanya shambulizi kali na kupata bao la kuongoza kupitia kwa Stéphane Sessegnon baada ya kupata pasi safi kutoka kwa Andre Wisdom.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog