Tuesday, December 17, 2013


MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Ureno, Cristiano Ronaldo amefungua jumba lake la makumbusho katika mji aliozaliwa ambapo amesema ameacha nafasi kwa tuzo ya Ballon d’Or na mataji mengine mengi atakayopata. Akiwa amesimama pembeni mwa tuzo yake ya Ballon d’Or aliyopata mwaka 2008 na tuzo zingine 125 alizopata peke yake au na timu tangu alipoanza kucheza soka, Ronaldo mwenye umri wa miaka 28 aliwaambia waandishi wa habari kuwa jumba hilo la makumbusho aliloliita CR7 ni zawadi kwa mashabiki wake. 
Ronaldo amesema anajivunia siku hiyo muhimu na pia ameacha nafasi kwa ajili ya tuzo zingine atazoshinda kabla hajaamua kutundika daluga rasmi. Shirikisho la Soka Duniani-FIFA limemtaja Ronaldo, Lionell Messi na Franck Ribery kugombea tuzo ya Ballon d’Or mwaka huu ambayo zamani ilikuwa ikijulikana kama tuzo ya mchezaji bora wa dunia wa mwaka.

Ronaldo na mpenzi wake Irina Shayk wakiingia kwenye jumba hilo linaloitwa  CR7
Golden boy: Ronaldo stands by a golden boot in the museum
Ronaldo stands by a golden boot in the museum
Scrum: Ronaldo addressed the media after the unveiling of his brand new waxwork
Ronaldo addressed the media after the unveiling of his brand new waxwork

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog