Tuesday, November 3, 2015


Kocha Mkuu wa Toto African, Martin Grelics akiagana na wachezaji wake baada ya mchezo na Azam FC kwenye Uwanja wa Chamazi. Kocha amevunja mkataba na timu hiyo.
Wachezaji wa Toto African wakiwa wamebeba ujumbe uliokuwa unasomeka 'Asante Sana Kocha Martin'
Beki wa Toto African, Salum Chuku (katikati) akichuana na mshambuliaji wa Azam FC, Didier Kavumbagu (wa pili kushoto) wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Chamazi jijini Dar es Salaam jana. Azam ilishinda 5-0.
KOCHA Mkuu wa Toto African ya Mwanza, Martin Grelics kutoka Ujerumani, ameamua kubwaga manyanga kuifundisha timu hiyo.
Martin alifikia uamuzi wake huo jana, muda mfupi baada ya Toto African kuchapwa mabao 5-0 na Azam katika mechi ya ligi kuu iliyochezwa kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar esSalaam.
Hakuna taarifa zaidi iliyotolewa kuhusu sababu za kocha huyo kubwaga manyanga,lakini wachambuzi wa masuala ya soka wameeleza kuwa, haridhishwi na usimamizi na uendeshaji wa timu hiyo.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog