Thursday, August 21, 2014


I'm out: Tim Sherwood has announced that he will not become the next Crystal Palace manager on Thursday
Mimi sipo!: Tim Sherwood jana ametangaza kuwa hatakuwa kocha Crystal Palace .

TIM Sherwood amejitoa mwenyewe katika mbio za kuwa kocha mpya wa Crystal Palace.
Kocha huyo wa zamani wa Tottenham Hotspur alikuwa anapewa nafasi kubwa ya kuteuliwa kuwa kocha mkuu wa Selhurst Park baada ya Malky Mackay kuondolewa katika kinyang'anyiro.
Lakini Sherwood hajavutiwa kurithi mikoba ya kocha aliyeondoka Tony Pulis, na hii inamaanisha Keith Millen ataendelea kuiongoza timu hiyo kwa muda katika mechi ijayo ya ligi kuu dhidi ya West Ham uwanja wa nyumbani.
No go: Sherwood is said to be uninterested in the job and has confirmed he will not take over as manager
Siendi: Sherwood anasema hajavutiwa na kazi hiyo na amethibitisha kuwa hatarithi mikoba.
"Palace ni klabu kubwa yenye utamaduni wake, lakini ipo katika hali ngumu ambayo haiwezi kuonekana kirahisi," Sherwood aliwaambia Sky Sports.
Makubaliano binafsi baina ya Sherwood na Palace yalishindwa kufikia muafaka baada ya kuripotiwa kuwa kocha huyo alitaka kuwa pamoja na wasaidizi wake wakati akiwa Spurs,  Chris Ramsey na Les Ferdinand katika dimba la Selhurst Park.
Mmiliki wa Palace, Steve Parish aligoma mapendekezo hayo na sasa anaangalia uwezekanao wa kupata kocha mpya zikisalia saa 48 tu klabu hiyo ijitupe uwanjani katika mchezo wa ligi kuu.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog