Thursday, August 21, 2014


1408543326669_wps_1_SAO_PAULO_BRAZIL_JULY_09_Walizinguana: Argentina Sergio Aguero na Marcos Rojo walitamkiana maneno makali katika fainali za kombe la dunia.
MECHI ya watani wa jadi nchini England baina ya Manchester United na Manchester City “The Manchester derby” itakuwa na ladha tofauti msimu huu ambapo nyota wawili wanaocheza timu ya taifa ya Argentina, Sergio Aguero na Marcos Rojo watakutana.
Wachezaji hao wawili waliocheza fainali ya kombe la dunia walisemekana kutamkiana maneno makali wakati wa mashindano ya majira ya kiangazi nchini Brazil baada ya Rojo ambaye amekamilisha kujiunga na Manchester United kwa paundi milioni 16 kutoka klabu ya Sporting Lisbon kumkaribisha rafiki yake, mkali wa muziki wa  Pop nchini Argentina, El Polaco ndani ya chumba cha kubadilishia nguo baada ya mchezo wa makundi.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog