Tuesday, September 15, 2015

Mashindano ya maarufu ya urembo duniani, Miss Universe, sasa yatakuwa chini ya kampuni ya kusaka, kuendeleza vipaji na masoko ijulikanayo kwa jina la WME/IMG. 
Awali mashindano hayo yalikuwa yakiendeshwa kwa ushirika baina ya kampuni hiyo na kampuni inayojishughulisha na masuala ya habari na burudani ya NBCUniversal na mtangazaji maarufu wa vipindi vya televisheni, mwanasiasa na mfanyabiashara, Donald J Trump. 
Akizungumza jijini jana, Mwandaaji wa mashindano ya Miss Universe Tanzania, Maria Sarungi Tsehai alisema kuwa wamepokea taarifa kuhusiana na kampuni mpya hiyo ambayo pia inaandaa mashindano ya Miss USA na Miss Teen Usa. 
Maria ambaye pia ni mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Compass Communications alisema kuwa wamepokea mabadiliko hayo na wataendelea kufanykazi na mmiliki huyo mpya ili kuendeleza vipaji vya wasichana nchini. 
Alisema kuwa mashindano ya Miss Universe ni moja kati ya matukio makubwa ya burudani duniani ambayo usaidia wasichana kutoka nchi zaidi ya 190 zinazoshiriki kila mwaka na watu zaidi ya nusu bilioni kufuatilia mashindano hayo kwa njia mbalimbali ikiwemo mitandao na televisheni. 
“Kwa sasa tupo katika maandalizi ya kufanya mashindano ya Miss Universe Tanzania, tunaamini kuwa mabadiliko haya yatatupa changamoto zaidi kwa lengo la kufika mbali na zaidi kuhakikisha tunatwaa taji baada ya matokeo mazuri ya Flaviana Matata ya mwaka 2007 ambapo aliingia hatua ya 10 bora,” alisema Maria. 
Afisa Mkuu wa kampuni ya WME/IMG, Mark Shapiro ameahidi kuyaendeleza mashindano hayo kufika ngazi ya juu kabisa ikiwa pamija na washindano bora. 
"Najisikia faraja kuendshs mashindano haya, tutayaendeleza kwa kiwango kikubwa na kuhakikisha umaarufu wake unaongezeka, naamini mashabiki wengi zaidi kwa sasa watafuatilia mashindano yetu kwa njia ya mbalimbali,” alisema Shapiro.
Maria Mwandaaji wa mashindano ya Miss Universe Tanzania, Maria Sarungi Tsehai alizungumza katika mashindano yaliyopita.
Miss Universe Tanzania 2014 Caroline Bernard akitoa elimu ya afya kwa wanafunzi wa kike katika shule ya msingi Msimbazi Mseto

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog