Tuesday, June 16, 2015


Wakala wa Fowadi wa Hoffenheim Roberto Firmino amethibitisha kuwa Mchezaji huyo anahamia England kwa ajili ya Msimu ujao.
Roger Wittmann, ambae anamwakilisha Nyota huyo mpya anaewika kutoka Brazil mwenye Miaka 23, amekataa kutoboa waziwazi ni Klabu ipi Mchezaji wake huyo atakwenda ingawa hivi karibuni amehusishwa na kujiunga na Manchester United.
Akiongea na Gazeti la Ujerumani, Bild, Wittmann amesema: "Ninachoweza kusema ni kuwa anahamia England!"
Hivi sasa Firmino yuko huko Nchini Chile akiwa na Timu ya Taifa ya Brazil inayocheza Fainali za Copa America, Kombe la Mataifa ya Marekani ya Kusini.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog