Monday, November 17, 2014


Tottenham Hotspur ina nia ya kumuuza Emmanuel Adebayor Mwezi Januari Dirisha la Usajili likifunguliwa baada ya Meneja wao Mauricio Pochettino kuamua kuipangua na kuisuka upya safu yake ya mashambulizi.
Chini ya Pochettino, Mchezaji huyo wa Kimataifa wa Togo ameshindwa kuonyesha cheche zake na hivi karibuni alikwaruzana na Mashabiki wa Tottenham.

Hata hivyo, chanzo cha habari hizi kimedai kuondoka kwa Adebayor kunaweza kuwa kugumu kutokana na Mshahara wake mkubwa wa Pauni 170,000 kwa Wiki ambao ni Klabu chache zinaweza kuumudu.
Emmanuel Adebayor

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog