Monday, September 1, 2014

Beki wa kati wa klabu ya Arsenal Laurent Koscielny ameondolewa katika kikosi chake cha cha timu ya taifa kwa sababubu ya majeraha ya kichwa yaliyompata baada ya hapo jana kugangana na mchezaji wa klabu ya Leicester City,Jeffrey Schlupp katika mchezo uliofanyika dimani King Power na timu zote kutoka sare ya goli 1-1.

View image on Twitter
Koscienly akipoke matibabu uwanjani mara baada ya kugongana kichwa na mshambuliaji wa Leicester City,Jeffrey Schlupp(hayupo katika picha) dimbani King Power ambapo timu zote zilitoka sare ya goli 1-1. 

Koscienly alipata jeraha hilo mnamo dakika ya 26 ya mtanange huo ambao nafasi yake ililazimika kuchukuliwa na Calum Chambers
Taarifa katoka shirikisho la soka nchini Ufaransa zimedhibitisha kuwa beki huyo kwa sasa hayupo katika hesabu ya wachezaji wa kikosi cha timu ya taifa kinachotarajia kucheza michezo miwili ya kirafiki siku za karibuni kati Hispania na Serbia.
Nafasi ya Koscienly kwa sasa katika kikosi cha timu ya taifa ya Ufaransa inaonekana kuchukuliwa na beki anayekipiga kunako klabu ya Barcelona Jeremy Mathieu.

Mathieu, amejiunga na Wakatalunya msimu huu akitokea Valencia na amekwisha fanikiwa kucheza michezo miwili ya kimataifa.

Kitengo cha utabibu ya klabu ya Arsenal kimesema kinaendelea na uchunguzi wa jeraha hilo kisha watasema rasmi ni kwa muda gani beki huyo atakuwa nje ya dimba akiuguza jeraha lake.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog