Monday, August 18, 2014


Diego Costa akishangilia bao lake...Andre Schürrle akipongezana na Diego Costa baada ya kufunga bao. Chelsea waliongoza kipindi hicho cha kwanza kwa kuwabamiza Wenyeji Burnley bao 3-1. Kipindi cha pili hakuna aliyeliona lango la Mwenzake licha ya timu zote mbili kushambuliana kwa zamu!Kipindi cha kwanza Dakika 14 Burnley walitangulia kufunga bao kupitia kwa Scott Arfield baada ya kutuliza vyema pasi ya Matthew Taylor ndani ya box na dakika 16 Chelsea wakasawazisha kupitia kwa Diego Costa...
Dakika ya 21 Chelsea waliongeza bao la pili kupitia kwa Andre Schürrle akilishwa mpira na Cesc Fàbregas. Bao la tatu lilifungwa na Branislav Ivanovic katika dakika ya 34 akipewa pasi tena na Cesc Fàbregas na kufanya 3-1 dhidi ya Wenyeji Burnley. VIKOSI: 
Burnley: Heaton, Trippier, Duff, Shackell, Mee, Taylor, Marney, Jones, Arfield, Ings, Jutkiewicz.
Subs: Wallace, Kightly, Sordell, Gilks, Long, Barnes, Dummigan.
Chelsea: Courtois, Ivanovic, Cahill, Terry, Azpilicueta, Fabregas, Matic, Schurrle, Oscar, Hazard, Costa.
Subs: Cech, Luis, Zouma, Torres, Drogba, Mikel, Willian.
Referee: Michael Oliver (Northumberland)
Mourinho akiteta jambo leo muda mfupi kabla ya MtanangeMourinho na Viongozi wenzake wakijiuliza jambo

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog