Thursday, July 17, 2014


Go west: Rio Ferdinand is set to join QPR after leaving Manchester United
Anaenda Magharibi: Rio Ferdinand anatarajia kujiunga na QPR baada ya kuondoka Manchester United.

Imechapishwa Julai 17, 2014, saa 6:46 mchana

BEKI mkongwe, Rio Ferdinand hatarithi mikoba ya unahodha wa Clint Hill katika klabu ya QPR mara atakapokamilisha uhamisho wake.
Ferdinand anamalizia taratibu za kujiunga na klabu hiyo ya Magharibi mwa London na anatarajiwa kusaini mkata muda wowote kutoka sasa.
Nahodha huyo wa zamani wa Manchester United na timu ya Taifa ya England yupo katika hatua ya mwisho ya makubaliano ya mkataba mwa mwaka mmoja na QPR baada ya kuondoka Old Trafford mwishoni mwa msimu uliopita.
New chapter: Ferdinand is set to join QPR
Ukurasa mpya: Ferdinand anataka kujiuna na QPR

Uhamisho huo utamkutanisha na kocha Harry Redknapp, ambaye alimsajili kwa mara ya kwanza akiwa mdogo katika klabu ya West Ham miaka 21 iliyopita.
 Redknapp alisema:"Ni dili kubwa. Rio atakuwa mchezaji mkubwa kwetu kutokana na maarifa na uzoefu wake katika  mchezo wa soka".
Licha ya uzoefu wake uwanjani, Redknapp hatampa unahodha klabuni hapo.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog