Thursday, July 17, 2014

article-2696004-1FB0265200000578-757_634x503Bosi mpya: Louis van Gaal alifanya mkutano wake wa kwanza na waandishi wa habari leo tangu ajiunge na Manchester United.
LOUIS van Gaal amesema Manchester United ni klabu kubwa duniani, lakini inatakiwa kujijenga upya baada ya kuvurunda msimu uliopita.
Van Gaal amefanya mkutano wake wa kwanza na waandishi wa habari tangu ajiunge na Man United baada ya kumaliza nafasi ya tatu ya kombe la dunia akiwa na timu ya Taifa ya Uholanzi.
Mholanzi huyo ameisifu klabu ya United kuwa ni kubwa katika ulimwengu wa soka, lakini aliwakumbuksha mashabiki kuwa maboresho ya haraka yanahitajika ili kuepukana na majanga waliyokumbana nayo msimu uliopita.
article-2696004-1FB9622500000578-188_634x356 
Gwiji wa zamani na gwiji ajaye? Louis van Gaal akitambulishwa kwa waandishi wa habari na  Sir Bobby Charlton.
“Msimu uliopita mlikuwa wa saba, kwahiyo ninyi sio klabu kubwa. Mnatakiwa kujithibitsha wenyewe,” alisema.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog