Friday, August 8, 2014



On the score sheet: Ryan Giggs slots home a goal in front of a 12,000 crowd to the AJ Bell Stadium but couldn't stop his side suffering a 5-1 defeat
Mtaalamu: Ryan Giggs alifunga bao pekee la kufutia machozi katika kichapo cha mabao 5-1.
Midfield maestro: Paul Scholes keeps his composure in game against the side he now co-owns one year after retiring from professional football
Kiungo mwalimu: Paul Scholes akimiliki mpira kuonesha kuwa ujuzi hauzeeki.
Wing wizard: Manchester United's new assistant manager Ryan Giggs performs a trademark dribble past Salford City opponent
Winga mchawi: Kocha mpya msaidizi wa Manchester United, Ryan Giggs akimpiga chenga mpinzani wake wa  Salford City
On managerial duties: Former Manchester United star Rio Ferdinand
Majukumu ya ukocha: Nyota wa zamani wa Manchester United, Rio Ferdinand

MAGWIJI wa Manchester United wale wa kikosi cha mwaka 1992 ‘Class of 92’ walishindiliwa kipigo kizito cha mabao 5-1 dhidi ya timu ya daraja la chini ya Salford City jana usiku.
Salford ni timu ambayo inamilikiwa na magwiji, Paul Scholes, Nicky Butty na Gary na Phil Neville.
Mchezo huo ulikuwa wa hisani na ulitazamwa na mashabiki  wapatao 12,00 katika dimba la Aj Bell Mjini Eccles.
Katika mchezo huo, Mkongwe Ryan Giggs ambaye kwa sasa ni kocha msaidizi wa Manchester United alimtamanisha kocha wake mkuu Louis Van Gaal kwa kufunga bao moja la kufutia machozi katika kipigo hicho cha mbwa mwizi.
Pamoja na kuzidiwa kasi na vijana wa timu hiyo kutokana na umri kuwa mkubwa, lakini nyota hao wa zamani wa Man United walionesha kiwango kizuri na kudhihirisha kuwa ujuzi hauzeeki.
Rio Ferdinand aliyesafiri kuwafundisha magwiji hao kama kocha msaidizi, alishindwa kuwanusuru na kichapo.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog