Thursday, August 7, 2014



MWANASHERIA wa Luis Suarez anajiamini kuwa adhabu ya kifungo cha miezi minne cha mshambuliaji wa Barcelona, Luis Suarez itapunguzwa na mahakama ya juu ya rufani ya michezo ya CAS ambapo rufani hiyo itasikilizwa kesho ijumaa.
Suarezi alikata rufaa kupinga adhabu ya kufungiwa shughuli zote za soka na FIFA na rufani yake itasikilizwa Agosti 8 mwaka huu katika mahakama hiyo iliyopo Lausananne, Uswizi.
Nyota huyo mwenye miaka 27 alifungiwa baada ya kumng’ata beki wa Italia,Giorgio Chiellini wakati akiichezea Uruguay katika mechi ya kombe la dunia nchini Brazil na baada ya tukio hilo alijiunga na Barcelona kwa ada ya uhamisho ya paundi milioni 75 kutokea Liverpool.
Rufani aliyowasilishwa FIFA na Suarez alitupiliwa mbali mwezi uliopita na akaamua kukata rufani mahakama ya juu ya rufani ya michezo.
Maamuzi ya CAS yanatarajia kutolewa wiki ijayo. Kama atashinda maana yake Suarez ataanza mazoezi na wachezaji wenzake wiki mbili zijazo na atakuwepo katika mechi ya ya kwanza ya msimu mpya wa La Liga dhidi ya Elche, jumapili ya Agosti 24 mwaka huu.
Shirikisho la soka la Uruguay (UAF) lilimteua wakili wa Brazil, Daniel Cravo ili asimamie rufani dhidi ya kifungo ambacho kimemfanya Suarez akose mechi 9 za kimataifa. Mchezo mmoja wa kifungo umepita ambao ulikuwa dhidi ya Colombia hatua ya 16 ya kombe la dunia.
Cravo aliiambia Radio Globo akiwa Brazil kuwa anaamini adhabu hiyo itapunguzwa.
“Nadhani FIFA walitaka kuonesha kuwa wanaweza kuchukua hatua,” alisema.” Maamuzi hayakuridhisha ukilinganisha na matukio makubwa yaliyowahi kutokea huko nyuma. Hata kifungo cha (Zinedine) Zidane mwaka 2006 au yale ya Leonardo na (Mauro) Tassotti mwaka 199, adhabu haikuwa kubwa zaidi”.
“Tukio la Suarez ndio baya zaidi kuwahi kutokea katika historia ya kombe la duniua?
“Naamni kifungo kitakachoathiri kazi yake kwa ngazi ya klabu kitaondolewa. Hakuna kesi iliyoamuriwa kama hiyo katika historia.

“Naenda kujaribu na kupunguza kifungo cha kuichezea Uruguay—mechi tisa ni nyingi sana na zinaweza kumzuia kucheza mpaka 2016

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog