Thursday, August 7, 2014


New: The Premier League have confirmed that referees will use vanishing spray this season
Mpya: Msimu ujao Ligi kuu nchini England imethibitisha matumizi ya dawa hii ya kupulizia.
BAADA ya kuthibitisha matumizi ya dawa maalumu ya kupulizia, ile inayokauka haraka na alitumiwa kombe la dunia, bodi ya ligi kuu England imeripotiwa kuagiza chupa 2,000 kwa ajili ya marefa msimu ujao, kwa mujibu wa gazeti za  Daily Telegraph.
Waamuzi watamaliza msimu ujao wakiwa na dawa hiyo ambayo itawasaidia kuweka alama umbali wa mita 10 kutoka kwenye mpira pale inapotokea adhabu ndogo na mabeki wanatakiwa kuweka ukuta.
Mkurugenzi mkuu wa ligi kuu, Richard Scudamore alisema: 'Tunaenda sambamba na maendeleo yanayoongeza ushindani na tulitazama kombe la dunia na kuona dawa ya kupuliza iliyotumika na waamuzi, hakika iliwasiaida marefa, wachezaji na wale wote waliokuwa wanaangalia mechi".

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog