Friday, August 8, 2014



1407452428918_wps_2_Manchester_City_FC_via_Pr
Manchester City wanamtaka Sergio Aguero asaini mkataba mpya kabla ya kuanza msimu mpya.
MANCHESTER City wanatumaini kuwa Sergio Aguero atasaini mkataba mpya utakaomfanya alipwe paundi laki mbili na elfu 10 kwa wiki kabla ya kuanza kwa msimu mpya.
Mabingwa hao wa England wameweka wazi kuwa mshambuliaji huyo wa Argentina yupo katika mipango yao ya baadaye pamoja na nahodha Vincent Kompayn na mazungumzo yanaendelea vizuri.
Barcelona na Real Madrid wameweka wazi siri ya kuvutiwa na mshambuliaji huyo mwenye miaka 26, lakini City wanafanya haraka ili kumuongezea mkataba wa miaka mitano.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog