Friday, August 8, 2014




azam-xi-v-yanga-11
KIKOSI cha pili cha mabingwa wa ligi kuu soka Tanzania bara, Azam fc kitakabiliana na Mtibwa Sugar katika mchezo wa kirafiki utakaopigwa leo katika Tamasha la Usiku wa Matumaini , uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Hii itakuwa mechi nzuri kwa timu zote kuangalia uwezo wa wachezaji waliowasajili na wale waliopandishwa kutoka timu za vijana.
Afisa habari wa Azam fc, Jafar Idd Maganga alisema wanauchukulia mchezo huo kwa uzito wa hali ya juu kwasababu ni nafasi nzuri kwa wachezaji wao kuonesha uwezo mbele ya timu bora ya Mtibwa Sugar.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog