Friday, September 4, 2015



Licha ya kuwa alishindwa kutamba katika klabu ya Manchester United kama ilivyokuwa matarajio ya wengi Dimitar Berbatov aliamua kutimkia katika klabu ya Fulham, AS Monaco na sasa kajiunga na klabu ya PAOK ya Ugiriki aliyojiunga nayo msimu huu.
2BF1729700000578-0-image-a-128_1441295520858
Mshambuliaji huyo wa Kibulgaria mwenye umri wa miaka 34 amejiunga na klabu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili akitokea katika klabu ya AS Monaco. Dimitar Berbatov ameingia katika usajili wa kihistoria wa klabu ya PAOK baada ya kusaini mkataba wa miaka 2.
2BF1722B00000578-0-image-a-126_1441295333059
Mara nyingi katika Ligi kubwa duniani mshambuliaji anayefanyiwa utambulisho maalum uwanjani ni yule mwenye jina kubwa pamoja na uwezo mkubwa uwanjani, licha ya Berbatov kuonekana kaisha uwanjani, kwa upande wa Ugiriki Septemba 3 ilikuwa ni siku yake maalum ya kutambulishwa mbele ya mashabiki 10000 katika uwanja wa Toumba.
2BF16D3600000578-0-image-a-127_1441295414401
0B8DC11B00000578-0-image-a-129_1441295673458
Dimitar Berbatov wakati yupo Man United

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog