Thursday, July 31, 2014


Mkurugenzi wa bendi, Isha Mashauzi akilikabili jukwaa vilivyo.
Bendi ya Taarab inayokimbiza mjini, Mashauzi Classic usiku wa kuamkia leo ilikamua kinoma katika ukumbi wa Lina's Night Club Bukoba Mjini. Kiongozi wa Mashauzi Classic, Isha Makongo akiliongoza kundi lake kutoa burudani katika Ukumbi wa Lina's Night Usiku huuBaadhi ya Waimbaji wa Kundi hilo la Mashauzi Classic wakiwajibika jukwaani kutoa burudani kwa Mashabiki wao.Kikosi kizima cha Mashauzi Classic kikifanya mashambulizi jukwaani.

Isha Makongo akiimba mbele ya Waimbaji wake Jukwaani kuwapa raha mashabiki wao wa bukoba usiku huu.
Hashim Said mwimbaji kiongozi msaidizi akifanya yake

Kundi la Mashauzi Classic Modern Taarab, usiku wa kuamkia leo liliwanogesha mashabiki wake katika onesho lililofanyika Ukumbi wa Lina's Night Club Bukoba na Kushuhudiwa na Watu wengi waliojitokeza kwa Wingi katika Ukumbi huu.
Mashabiki wa bendi hiyo wakiburudika kwa nyimbo za Taarab kutoka kwa Bendi hiyo ya Mashauzi Classic kwa  raha zao.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog