Thursday, March 13, 2014


Rais wa Shirikisho la soka duniani, FIFA Sepp Blatter, ameelezea wasi wasi wake kuhusiana na maandamano yanayoendelea nchini Brazil, huku taifa hilo likijiandaa kuwa mwenyeji wa kombe la dunia. Kwa mara ya kwanza katika historia ya FIFA, Blatter amesema hakutakuwepo kwa hotuba wakati wa sherehe za ufunguzi. Katika mahojiano na jarida moja la Ujerumani, Blatter amesema anatarajia kuwa fainali hizo zitasaidia kutuliza hali ya kisiasa nchini Brazil. Mwaka uliopita rais wa Brazil, Dilma Rousseff, alizomewa na mashabiki wa soka wakati wa sherehe za ufunguzi za kombe la Shirikisho, ambalo hutumiwa na FIFA kama maandalizi ya mwisho kabla ya kuanza kwa kombe la dunia. Waandamanaji waliandamana katika barabara za miji mingi kabla na baada ya fainali hizo za kombe la Shirisho, wakipinga ufisadi na gharama za kuandaa fainali hizo za dunia.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog