Thursday, March 13, 2014

ks flu 
Msafara wa Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara timu ya Young Africans leo asubuhi umeondoka jijini Dar es salaam kuelekea mjini Morogoro tayari kwa mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar siku ya jumamosi, mechi itakayopigwa kwenye dimba la Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Young Africans inayonolewa na makocha Hans Van der Pluijm kutoka Uholanzi, Charles Mkwasa na Juma Pondamali wazawa jana jioni ilifanya mazoezi katika Uwanja wa Kaunda ikiwa ni masaa 10 baada ya kuwasili kutokea jijini Cairo ilipocheza dhidi ya Al Ahly katika mashindano ya Klabu Bingwa barani Afrika.
Kuhusu mchezo wenyewe Kocha Hans amesema haifahamu vizuri timu ya Mtibwa Sugar lakini kwa kushirikiana na wenzake wamejiandaa kuhakikisha timu inafanya vizuri na kupata pointi 3 katika mchezo huo, yaliyotokea Misri yameshapita sasa kilichobakia ni kutetea Ubingwa wa Ligi Kuu.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog