Thursday, March 13, 2014

 

loga maelezo 
Kocha wa Simba SC, Mcroatia, Dravko Logarusic akitoa maelekezo kwavijana wake
Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe, Dar es salaam
0712461976 au 0764302956
WEKUNDU wa Msimbazi Simba wamelaumu timu zinazoingia kwa kukamia wapinzani wao katika mitanange ya lala salama ligi kuu soka Tanzania bara msimu wa 2013/2014.
Akizungumza na mtandao huu, afisa habari wa Simba Asha Muhaji amesema hali ya kukamiana uwanjani inaharibu ubora wa mpira katika mechi mbalimbali.
“Kuna wakati unaweza kushangaa, mchezaji fulani akawa na kazi ya kumkaba kwa nguvu mshambuliaji wenu. Mfano Amissi Tambwe kwa Simba, badala ya kucheza mpira kwa ufanisi, yeye anacheza kimabavu na kumjeruhi mwenzake. Sasa mpira kama huu hauna maana”. Alisema Asha.
 

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog