Thursday, March 13, 2014

SIMBASC21 

WEKUNDU wa Msimbazi Simba wamelaumu timu zinazoingia kwa kukamia wapinzani wao katika mitanange ya lala salama ligi kuu soka Tanzania bara msimu wa 2013/2014.
Akizungumza na mtandao huu, afisa habari wa Simba Asha Muhaji amesema hali ya kukamiana uwanjani inaharibu ubora wa mpira katika mechi mbalimbali.
“Kuna wakati unaweza kushangaa, mchezaji fulani akawa na kazi ya kumkaba kwa nguvu mshambuliaji wenu. Mfano Amissi Tambwe kwa Simba, badala ya kucheza mpira kwa ufanisi, yeye anacheza kimabavu na kumjeruhi mwenzake. Sasa mpira kama huu hauna maana”. Alisema Asha.
Asha aliongeza kuwa kukamia mechi kwa kucheza mpira mzuri hakuna tatizo kwani kila timu kwa sasa inahitaji ushindi, lakini kukamiana kwa kuumizana si jambo zuri.
“Kuna timu zinahitaji ubingwa au nafasi nzuri za juu, vilevile kuna timu zinakwepa kushuka daraja. Mazingira haya yameifanya ligi iwe ngumu sana. Lakini tatizo ni uchezaji wa ubabe kwa baadhi ya timu. Kuumia ni kawaida katika mpira, lakini kuna mazingira mengine yanatokana na kukamiana”. Alisema Asha.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog