Friday, July 18, 2014


Moving on: Luis Suarez, signs Uruguay shirts and flags and throws them back to fans outside his house
 Luis Suarez, alitia muhuri katika jezi na bendera ya Uruguay na kuwatupia mashabiki nje ya nyumba yake.

Imechapishwa Julai 18, 2014, saa 11:07 jioni

BARCELONA inatarajia kumpa majukumu mpya nyota wake Lionel Messi ambapo sasa atacheza nyuma ya washambuliaji wawili, Luis Suarez na Neymar, kwa mujibu wa ripoti za Hispania.
Kuelekea msimu ujao, Kocha Luis Enrique anataka kuwatumia washambuliaji wote watatu kwa wakati mmoja ndani ya kikosi chake.
Enrique anaamini kumhamisha Messi katika nafasi aliyozoeleka kucheza na kumchezesha nyuma upande wa kulia, kutawafanya Suarezi na Neymar wang`are zaidi. 
Lionel Messi is set for a new role at Barcelona
Lionel Messi is set for a new role at Barcelona
Mabadiliko: Lionel Messi anatarajiwa kupewa majukumu mapya katika klabu yake ya Barcelona, sasa atacheza nyuma ya Suarez na Neymar.

Main man: Neymar will join Suarez in attack after the Brazil star recovers from his fractured vertebra
Mtu muhimu: Neymar ataungana na Suarez kuongoza safu ya ushambuliaji ya Barcelona baada ya kupona majeruhi yake ya kuvunjika mfupa wa uti wa mgongo.
Suarez amefungiwa mpaka mwezi oktoba mwaka huu kwa kitendo cha kumng`ata beki wa Italia , Giorgio Chiellini  kwenye mechi ya makundi ya kombe la dunia nchini Brazil.
Baada ya kitedo hicho aliamua kuondoka Liverpool na kujiunga na Barca kwa ada ya uhamisho ya paundi milioni 75.
Wakatalunya wanasemekana kuanza harakati za kukata rufani juu ya adhabu hiyo.
Barcelona pia wanamsubiri Neymar apone majeruhi yake aliyoyapata kombe la dunia  hatua ya robo fainali.
Taifa mwenyeji bila Neymar lilipigwa mabao 7-1 kwenye mechi ya nusu fainali dhidi ya Ujerumani.
Wakati huo huo, Messi alitajwa kuwa mchezaji bora wa mashindano licha ya Argentina kufungwa bao 1-0 dhidi ya Ujerumani katika mechi ya kfainali.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog