Tuesday, July 22, 2014


RASMI Real Madrid wamekamilisha kumsajili mfungaji bora wa kombe la dunia, James Rodriguez kutoka klabu ya Monaco.
Nyota huyo wa kimataifa wa Colombia amekubali kusaini mkataba wa miaka sita na alichukuliwa vipimo vya afya  leo asubuhi na atatambulishwa jioni hii.
Hakuna klabu yoyote iliyothibitisha ada ya uhamisho ya mchezaji huyo mwenye miaka 23, lakini ripoti zinasema Madrid wamelipa paundi milioni 60 zitakazomuweka Rodrigues kuwa mchezaji namba nne katika orodha ya wachezaji ghali zaidi duniani.
Mchezaji ghali zaidi duniani ni Gareth Bale, akifuatiwa na Cristiano Ronaldo na Luis Suarez.
Done deal: James Rodriguez underwent his medical in Madrid and is set to be unveiled on Tuesday
Dili limekamilika: James Rodriguez alipimwa afya leo asubuhi.
Thumbs up: Rodriguez becomes the fourth most-expensive signing in history for £60million
Hapa dole sasa!: Rodriguez anakuwa mcheza namba nne katika orodha ya wachezaji ghali zaidi duniani 
Done: Rodriguez leaves the hospital Sanitas La Moraleja after his medical in Madrid
Tayari: Rodriguez akiondoka katika hospitali ya le Sanitas La Moraleja baada ya kupima afya mjini Madrid.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog