Thursday, May 8, 2014

486618_545707472135474_901587883_n
TAYARI mchakato wa uchaguzi katika klabu ya Simba sc umeshaanza  na tayari  mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi, Damas Ndumbaro ametangaza kuwa juni 29 mwaka huu uchaguzi utafanyika
Wapo watu wengi wanaotamani kuiongoza klabu ya Simba ambayo kwasasa ipo katika hali ngumu kwa soka la uwanjani.
Kumaliza nafasi ya nne nyuma ya Mbeya City, Yanga na Azam fc ni jambo linalowaumiza wana Simba wote.
Ni msimu wa pili mfufulizo Simba wanakosa nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa. Kwa ukongwe wake ni jambo la fedheha kubwa japokuwa mpira uko hivyo.
Hatuwezi kuwakosoa Simba kwa matokeo waliyokuwa wanapata kwasababu mpira wa miguu huwa unabadilika, lakini makosa yanapotokea kwasababu ya watu fulani kutowajibika, hapo lazima ukosoaji uhusike.
Kwa mfano wachezaji kushindwa kucheza vizuri kwasababu hawajalipwa posho na mishahara, unashindwaje kuukosoa uongozi kwa kushindwa kuwajibika?
Kumekuwapo na mivutano ya muda mrefu baina ya mwenyekiti wa Simba, sasa Rais, Ismail Aden Rage na  baadhi ya wajumbe wake wa kamati ya utendaji pamoja na baadhi ya wanachama.
Sinema nyingi zimeonekana na zimeandikwa, kila mtu anafahamu yaliyokuwa yanatokea Simba sc

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog