Thursday, May 8, 2014



Edin Dzeko akishangilia vikali baada ya kuifungia bao mbili City na kupanda kileleni usiku huu. Mtanange wao wa mwisho kuamua nani Bingwa kati yao na Liverpool, Huku Ushindi wa City wa bao 4-0 ukiwakalisha kileleni na pointi zao 83 na Liverpool wakishika nafasi ya pili wakiwa na pointi 81.

Dzeko hapa aliwaunganisha wachezaji wa City kwa pamoja na kumpongeza.Edin Dzeko
Kipindi cha kwanza kilimalizika wote wakiwa 0-0. Kipindi cha pili dakika ya 64 Manchester City walifanya mashambulizi na hatimaye Edin Dzeko kuipachikia bao la kwanza kwa kufanya 1-0 dhidi ya Aston Villa baada ya Dzeko kupata krosi iliyowapita mabeki ikipigwa na Pablo Zabaleta.Pleading: Joe Hart reacts as his side move within inches of the Premier League title
Dakika ya 72 tena Edin Dzeko aliifungia bao la pili na kufanya 2-0 dhidi ya Aston Villa. Bao la tatu lilifungwa na Stevan Jovetic akipewa pasi safi na Yaya Toure, Huku bao la Mwisho likifungwa na Yaya Touré katika dakika za majeruhi baada ya kuwachomoka wachezaji mabeki wa Aston Villa.Vincent Kompany
Yaya Toure alikokota Mpira toka Nusu yake ya Uwanja na kutembea nao  Mchezaji mmoja baada ya mwingine wa Villa na kupachika Bao la 100 la Ligi kwa City Msimu huu kitu ambacho hakijafanyika kwenye Ligi ya Juu England tangu Miaka ya 1950.Making his point: Paul Lambert shouts instructions to his side from his technical area
Nafasi pekee na safi waliyopata Villa ya kufunga ni pale Kichwa cha Weimann kugonga Posti ya Juu na kudunda chini nje ya Mstari wa Goli na kumwacha Mshambuliaji huyo asiamini nini kimetokea.
Ligi Kuu Engand inamalizika Jumapili kwa City kucheza Nyumbani na West Ham na wanahitaji Pointi 1 tu kutwaa Ubingwa labda Liverpool washinde, huku City wakitoka Sare, na kufuta Tofauti ya Mabao 13 ya City au City wafungwe Mechi hiyo na Liverpool kushinda.
Mechi ya Leo pia imefuta kabisa matumaini ya Chelsea kutwaa Ubingwa.
Can't even watch: Manuel Pellegrini can barely look with his side on the brink of a Premier League titleKocha wa City Manuel PellegriniAcrobatic: City captain Vincent Kompany attempts an audacious overhead kick
VIKOSI:
Man City: Hart, Zabaleta, Kompany, Demichelis, Kolarov, Javi Garcia, Toure, Milner, Silva, Nasri, Dzeko. 

Subs: Richards, Lescott, Negredo, Clichy, Fernandinho, Pantilimon, Jovetic.
Aston Villa: Guzan, Lowton, Vlaar, Baker, Clark, El Ahmadi, Westwood, Delph, Weimann, Bowery, Bertrand. 
Subs: Bacuna, Steer, Sylla, Tonev, Holt, Robinson, Grealish.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog