Wednesday, January 29, 2014


Mechi kati ya Liverpool na Everton
Klabu ya Liverpoool inaendeleza kampeni yake ya kutaka kuwa miongoni mwa timu nne bora katika Ligi Kuu ya England baada ya kuichachawiza Everton mabao 4-0 katika mchuano wa katikati ya juma ulioandaliwa Jumanne katika uwanja wa Anfield.
Mechi hiyo ilitajwa kama muhimu zaidi kuwahi kushirikisha pande hizo mbili baada ya kipindi cha miaka 30.
Liverpool ilitangulia kuzibusu nyavu za Everton mapema kuvuna mabao matatu; moja kupitia mkwaju wa kichwa kutoka kwa Steven Gerrad na huku Daniel Sturrige akifuma mabao mawili dakika tatu baadaye..
Everton ilipata pigo baada ya mshambulizi wa kutegemewa Romelu Lukaku kuondoka uwanjani juu ya machela baada ya kupata jeraha la kiwiko cha mguu. Aligongwa vibaya na Gareth Barry alipokuwa akijaribu kumnyima Steven Gerrard fursa ya kufunga bao.
Rodgers apongeza "juhudi kuu" za Liverpool
Ushindi huo mnono wa Liverpool tangu November 1982 umekiwezesha kikosi hicho cha Brendan Rogers kujipiga kifua juu ya matumaini ya kulidaka taji la ligi kuu. Brendan Rogers amesifu juhudi kubwa za wachezaji wake.
Katika matokeo ya mechi nyinginezo Manchester United iliishinda Cardiff mabao 2-0, Norwitch City na New Castle United zikatoka sare ya kutofungana, nao viongozi wa ligi Arsenal wakapata pigo katika kampeni yao kwa kulazimishwa kutoka sare ya mabao 2-2 ugenini dhidi ya Southampton.
Swansea iliichabanga Fulham 2-0, Crystal Palace 1 Hull 0 na Liverpool.
Leo Jumatano Manchester City itashuka dimbani ugenini kutafuta alama za kushika usukani kwenye jedwali dhidi ya Totteham Hotspurs, Aston Villa watamenyana na West Brom, Chelsea itaialika West Ham, Sunderland itaikaribisha Stoke.

UNAMFAHAMU ASKOFU ANAEISHI KAMA RAIS HAPA BONGO??!!.. MSAFARA WAKE UNAGHARIMU ZAIDI YA SHILING MILIONI 200


Maisha ya Askofu wa Huduma ya Ngurumo ya Upako, Geor Davie anayevuma zaidi jijini Arusha na Dar es Salaam ni ya kifahari, anaabudiwa zaidi ya manabii na analindwa kuliko marais mbalimbali duniani.

Davie ambaye hujulikana zaidi kwa jina la Mtume, ana msafara mrefu kwenye ziara zake anazokwenda kutoa huduma ambao husheheni magari mengi ya kifahari kuliko marais wengi.
OneloveTz tuna mlolongo wa matukio ya Davie ambayo yanajieleza kwa picha ambazo zinabainisha namna mtumishi huyo wa Mungu anavyokula bata.

MSAFARA WA SHS. MIL. 200
Matukio yanaonesha kuwa, baadhi ya misafara ya Davie imekuwa na msururu mrefu wa magari ambayo hayapungui kumi.

Uchunguzi umeonesha kuwa, magari hayo, kila moja linanunuliwa kati ya shilingi milioni 20 na 40, hivyo thamani ya ‘mikoko’ peke yake inaleta wastani wa jumla ya zaidi ya shilingi milioni 200 bila ya mafuta ambayo nayo hugharimu fedha nyingi.

ULINZI DAH!
Kila sehemu ambayo Davie hufika kwa lengo la kutoa huduma, huzungukwa na walinzi kati ya nane na 10 ambao huvaa nadhifu, suti nyeusi na miwani nyeusi.

Walinzi hao, humzunguka Davie na kufanya anapotembea asikaribiwe na watu kwa urahisi, huku wakimuongoza hatua kwa hatua.

Habari zinadai kuwa walinzi hao wameajiriwa na Kanisa la Huduma ya Ngurumo ya Upako na hulipwa mishahara kwa ajili ya kumlinda kiongozi huyo.

GARI LAKE LINA BENDERA MBILI
gari la Davie ambalo hupambwa na bendera mbili kama ilivyo kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa kawaida, gari la rais hupambwa na bendera mbili, moja ikiwa ya taifa na nyingine ya rais.
Hata hivyo, blog hii halijapata ufafanuzi kuhusu bendera mbili za gari la Davie, ingawa waumini wake wanasema kwamba ni alama ya huduma ya kanisa lake.

NI RED CARPET KILA ANAPOKWENDA
Davie anaheshimiwa kwa kiasi kikubwa na waumini wa huduma ya kanisa lake, hivyo hutandikiwa zulia jekundu ‘red carpet’ kila anapokwenda kutoa neno, huku akizungukwa na walinzi wake.

FULL KUABUDIWA
Neno la Davie siyo tu kwamba linampa wafuasi bali pia kwa wengine humuabudu kwa imani kuwa amejaliwa ufunuo mkubwa wa matatizo ya binadamu aliopewa na Mwenyezi Mungu.
blog hili lina picha za watu wakisujudu na kumshika viatu kwa imani kwamba tendo hilo huwapa utakaso wa kiroho na matatizo mbalimbali.


UNAMFAHAMU ASKOFU ANAEISHI KAMA RAIS HAPA BONGO??!!.. MSAFARA WAKE UNAGHARIMU ZAIDI YA SHILING MILIONI 200


Maisha ya Askofu wa Huduma ya Ngurumo ya Upako, Geor Davie anayevuma zaidi jijini Arusha na Dar es Salaam ni ya kifahari, anaabudiwa zaidi ya manabii na analindwa kuliko marais mbalimbali duniani.

Davie ambaye hujulikana zaidi kwa jina la Mtume, ana msafara mrefu kwenye ziara zake anazokwenda kutoa huduma ambao husheheni magari mengi ya kifahari kuliko marais wengi.
OneloveTz tuna mlolongo wa matukio ya Davie ambayo yanajieleza kwa picha ambazo zinabainisha namna mtumishi huyo wa Mungu anavyokula bata.

MSAFARA WA SHS. MIL. 200
Matukio yanaonesha kuwa, baadhi ya misafara ya Davie imekuwa na msururu mrefu wa magari ambayo hayapungui kumi.

Uchunguzi umeonesha kuwa, magari hayo, kila moja linanunuliwa kati ya shilingi milioni 20 na 40, hivyo thamani ya ‘mikoko’ peke yake inaleta wastani wa jumla ya zaidi ya shilingi milioni 200 bila ya mafuta ambayo nayo hugharimu fedha nyingi.

ULINZI DAH!
Kila sehemu ambayo Davie hufika kwa lengo la kutoa huduma, huzungukwa na walinzi kati ya nane na 10 ambao huvaa nadhifu, suti nyeusi na miwani nyeusi.

Walinzi hao, humzunguka Davie na kufanya anapotembea asikaribiwe na watu kwa urahisi, huku wakimuongoza hatua kwa hatua.

Habari zinadai kuwa walinzi hao wameajiriwa na Kanisa la Huduma ya Ngurumo ya Upako na hulipwa mishahara kwa ajili ya kumlinda kiongozi huyo.

GARI LAKE LINA BENDERA MBILI
gari la Davie ambalo hupambwa na bendera mbili kama ilivyo kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa kawaida, gari la rais hupambwa na bendera mbili, moja ikiwa ya taifa na nyingine ya rais.
Hata hivyo, blog hii halijapata ufafanuzi kuhusu bendera mbili za gari la Davie, ingawa waumini wake wanasema kwamba ni alama ya huduma ya kanisa lake.

NI RED CARPET KILA ANAPOKWENDA
Davie anaheshimiwa kwa kiasi kikubwa na waumini wa huduma ya kanisa lake, hivyo hutandikiwa zulia jekundu ‘red carpet’ kila anapokwenda kutoa neno, huku akizungukwa na walinzi wake.

FULL KUABUDIWA
Neno la Davie siyo tu kwamba linampa wafuasi bali pia kwa wengine humuabudu kwa imani kuwa amejaliwa ufunuo mkubwa wa matatizo ya binadamu aliopewa na Mwenyezi Mungu.
blog hili lina picha za watu wakisujudu na kumshika viatu kwa imani kwamba tendo hilo huwapa utakaso wa kiroho na matatizo mbalimbali.

- See more at: http://onelovetz.blogspot.com/2014/01/unamfahamu-askofu-anaeishi-kama-rais.html?utm_source=feedburner&utm_medium=feed&utm_campaign=Feed%3A+blogspot%2FhgdRs+%28Onelove+Tz%29&utm_content=FaceBook#sthash.a37k9DV2.dpuf
- See more at: http://onelovetz.blogspot.com/2014/01/unamfahamu-askofu-anaeishi-kama-rais.html?utm_source=feedburner&utm_medium=feed&utm_campaign=Feed%3A+blogspot%2FhgdRs+%28Onelove+Tz%29&utm_content=FaceBook#sthash.a37k9DV2.dpuf

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog