Sunday, July 12, 2015


Makamba 1
January Makamba ni miongoni mwa waliojitokeza kuomba ridhaa ya chama cha mapinduzi CCM kuteuliwa kukiwakilisha chama kwenye kugombea Urais wa Tanzania 2015 ambapo alitajwa kwenye mchujo wa kwanza wa tano bora pamoja na Bernard Membe, Amina Salum, Asharose Migiro na John Magufuli.
Ilipofika time ya tatu bora alipata taarifa kwamba hajapita kwenye mchujo wa kwanza ambapo sekunde chache baadae aliandika yafuatayo >>> ‘Matokeo rasmi ya wana-CCM watatu watakaondelea na mchakato yatatolewa punde. Hatumo. Lakini nina fahari kubwa na kampeni yetu na timu yetu’
WATATU CCM
Orodha ya tatu bora ambayo mmoja wao atatangazwa kesho kuibeba bendera ya CCM.
Hatujapoteza uchaguzi kwasababu mimi na vijana niliokuwa tumejifunza mengi na tumejenga undugu. Tumepambana na matakwa ya Mungu yametimia, nawashukuru wote mliotuunga mkono. Mlitupa nguvu. Nawashukuru pia mliotupinga na kutukosoa. Mlitusaidia kujitazama na kujirekebisha‘ – January Makamba

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog